HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 26.

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 26. Ilipoishia.......... Alipomgeuza tu alishangaa kuona sura ya yule binti ni ya mbuzi. Aliogopa na kudondoka chini kwa kelele kuu alilia 'maaamaaaaaaa!!!!" Alijiokotaokota huku akiangukaanguka mpaka kwenye gari yake. Alipanda ndani ya gari na kuwasha gari. Alikimbiza gari mpaka akafika karibu na geti la nyumba ya Elvine, lakini kabla hajafika getini alishangaa kuona anaguswa mabegani ndani ya gari lake. Alitoa macho kwa uoga na mshtuko mkubwa mpaka akakosea njia na kwenda kugonga mti... Kusoma sehemu ya 25 bonyeza hapa. Sasa inaendelea......, Aligonga mti kwa nguvu mpaka naye akajipigiza kichwa kwenye usukani wa gari na gari ikaharibika sana upande wa mbele, alipona kwa neema tu kwa namna gari ilivyokuwa mwendo kasi angeweza hata kupoteza maisha lakini haikuwa hivyo. Alijikaza na kushuka kwenye gari akakimbia kuelekea kwenye nyumba ya Elvine,  njiani alikumbwa na kimbunga cha ajabu sana. Baada ya kile kimbunga kumpitia na kumzingazinga kwa muda

MUDA WA KUINGIA NA KUTOKA (ENTRY AND EXIT TIME).

 

                            MUDA WA KUINGIA NA KUTOKA (ENTRY AND EXIT TIME).

Kwa kila jambo kuna muda na majira yake.Nadhani kila mmoja wetu angalau alisha wahi kusafiri kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine.Inawezakuwa ndani ya wilaya au nje ya wilaya,ndani ya mkoa au nje ya mkoa,ndani ya nchi au nje ya nchi,kama ndiyo kweli utakubaliana na mimi kuwa,kuna wakati ulianza safari yako na kuna wakati uliimaliza safari yako.Hapo ndipo kusema kunawakati wa kuanza safari na wakati wa kuimaliza safari yako.Chukulia hata katika kusoma aidha shule ya msingi,shule ya sekondari,shule ya upili,Chuo cha kati au Chuo kikuu,utagundua kuwa kuna muda watu huingia kujiunga na masomo na kuna muda watu huhitimu masomo yao.

Vivyo hivyo kwa wakulima kuna muda wa kupanda na kuna muda wa kuvuna.Hii yote hutokea angalau kwa kila jambo kuwa na wakati wa kuanza na wakati wa kumaliza ndiyo maana kuna wakati ulizaliwa na kuna wakati utakufa.Sikutishii lakini ndivyo ilivyo na huo ndio uhalisia ya kuwa kila kitu kina wakati wa kuanza kwake na wakati wa kumalizika.Na haiwezi kutokea kuwa ukianza ndiyo umeanza hapana,lazima kuna wakati utafikia mwisho tu.Kwa mfano ukichukulia mfano wetu hapo juu wa kusafiri,wakati umepanda gari haukusafiri muda wote kuna wakati ulifika ukashuka kwasababu wakati wa kushuka ulikuwa umefika.

Rafiki hivi unajua ya kuwa muda unazungumza? Mfano,ukilala wakati wa kuamka ukifika,hata bila kuamshwa utaamka tu.Ukishindwa kufahamu nyakati na majira katika Maisha yako utapata tabu sana. Kuna wakati mwingine unaweza  kupishana na gari la mshahara kabisa .Hivyo wakati unaongea tena muda mwingine unakusemesha hata huna habari, ndiyo maana Mungu anaweza kukuletea watu fulani watakao saidia kusukuma mbele hatima ya maisha yako(destiny helper) lakini usiwatambue na wakati mwingine waliletwa ili wakuvushe katika hatua moja au nyingine na watu hawa usipo watambua kwa wakati sahihi unaweza kuja kuwagundua wakati ulishaenda na isikufae tena.

Wakati mwingine inaweza kuwa ni fursa ambayo imekuja mbele yako tena imekuja kwa wakati sahihi kabisa, inaweza ikawa ni kujifunza jambo fulani na wewe usiielewe wala kuchukua hatua yeyote.Utashangaa ukija kuielewa fursa hiyo wakati wake wa kutoka(exit time) ukawa umeshafika na usiifaidi tena.Na,hii hutokana na kutokujua wakati wa kuingia na kutoka kwa kitu fulani au wewe mwenyewe katika kitu fulani.

Nakumbua nilipokuwa nyumbani nilikutana na mama mmoja aliyekuwa akiuza Mchicha nilimuuliza kuwa anamuda gani anauza mchicha? Alijibu na kusema ana miaka kama nane hivi.Nikamwambia  woow! muda mrefu sana kumbe utakuwa ushajenga na nyumba tayari eeh? Akasema hapana,sababu alikuwa akikutana na changamoto nyingi sana na ilifika wakati aliamua kujiingiza kwenye kilimo lakini hakufanikisha chochote na matokeo yalikuwa yanafeli tu kila mara.Kwani kila alipo lima aidha mvua haikunyesha kabisa mwaka huo au maji kuzidi na kubeba mazao yake yote,na wakati huo anakuwa ametumia gharama kama zote.Nilimpa pole na kuuliza shida nini? Akasema hata yeye hakuelewa sababu ilikuwa nini.Lakini ilifika kipindi akakata tamaa kabisa na kuamua kuto kulima tena.Hivyo akaamua kufungua mgahawa kwaajili ya kujikimu yeye na familia yake.Pamoja na hayo mgahawa  haukuendelea na alishindwa kuuendesha kutoka na mtaji kuwa finyu,huku pesa nyingine ikitumika nyumbani kwa matumizi ya Nyumbani.Matokeo yake alijikatia tamaa na kurudi kwenye hiyo biashara yake ya kutembeza mchicha,hakutaka tena kusikia habari za kilimo.Ilipokuwa mwaka 2021 Mchungaji wake akamwambia alime Mpunga kwamaana mashamba yenyewe yalikuwa yanapatikana kwa bei ya chini sana,alikuwa amekata tamaa katika kilimo na hakutaka kusikia habari hizo kabisa,huwezi amini wakati mwingine mchungaji wake alikuwa akimkopesha hadi pesa na kumtafutia shamba ili tu alime,lakini hakutaka kusikia habari hizo.Mavuno ya mwaka huo yalikuwa mengi kuliko kawaida huku bei yake ilipanda mara tano zaidii.Mama huyo aliishia kujilaumu kwanini hakulima na alikataa hadi msaada kutoka kwa mchungaji wake.Basi akasema siyo mbaya akafanya harakati za kulima tena  mwaka uliofuata lakini mpunga wake ulipigwa na maji wote.

Unaweza kusema huyu mama alikuwa amelogwa vile au alikuwa na mkosi lah!,ni kwa namna tu hakujua wakati wake ni upi na pengine angelima mwaka 2021 ndiyo ingekuwa wakati wake wa kutoka kwake lakini hakulitambua hilo na aliamua kubaki kulaumu tu muda wote na kusema Maisha hayako fair kabisa.

Ngoja tumtazame jamaa mjoja anayejulikana kama Christopher Michael Langan, mtu huyu alikuwa na IQ kubwa sana iliyokadiriwa kuwa 195-210  kuliko hata ile ya Albert Einstein ambaye yeye ilikadiriwa kuwa 160 tu, yaani kwa ufupi alikuwa jiniazi.Mwaka 1999 alitajwa na waandishi wengi kuwa ni "the smartest man in America" or "in the world".Mwaka 2008 Kuna siku alikuwa anashiriki mashindano ya maswali na majibu ambayo yalikuwa yanafanyika kati ya watu 100 wenye akili sana kushindana na mtu mmoja yaani (1 VS 100).Hapa swali lilikuwa linaulizwa kisha pande mbili hizi zinashindana kujibu au kutoa jibu sahihi kwa haraka na upande wowote utakao jibu swali utalipwa pesa.Ikumbukwe upande mmoja ulikuwa na watu mia moja ambao wako vizuri kichwani na upande mwingine ulikuwa na mtu mmoja tu,ambaye siku hiyo ndiyo alikuwepo Langani ziidi ya hao wengine 100.Ningekupa historia ya Christopher Langan au basi goja tufanye wakati mwingine,ilikuwa ni kawaida nchini marekani kutokea kwa mashindano kama haya. Ajabu ni kuwa kila swali likiulizwa Langan alikuwa analifahamu na alijibu kwa haraka na kuwaacha wapinzani wake wakinong’ona kujadili jibu.Langan alivuna pesa nyingi sana kiasi cha dola za kimarekani 250,000 ambzo ni sawa na Tsh 587,500,000.Watu walimshangilia sana Langan lakini alipofikisha kiasi cha shilingi 587,500,000 aliamua kuinuka na kuondoka katika mashindano hayo.Watu walishangaa sana kuona akiondoka wakati alikuwa na uwezo wa kujibu maswali yote yaliyofuata na kupata pesa nyingi zaidi.Alipoulizwa akajibu na kusema “I know my entry and exit time”,yaani nafahamu muda wa kuingia na muda wa kutoka sasa yanipasa kuondoka  kwani huu ndiyo wakati wangu wa kuondoka hapa.

Kuna mengi ya kujifunza kutoka kwa Christopher Langan lakini yatupasa kutafakari na kuyafanyia kazi.

Hivi unafahamu kunawakati wa kuingia na kutoka katika kila unachokifanya? Hivi unafahumu kuwa kunawakati wa kuingia na kutoka kwenye mitandao ya kijamii? Kuna wakati wa kuingia na kutoka kwenye ajira? Hivi unajua kuwa kuna muda wa kuingia na kutoka kwenye hiyo fursa? Tambua sasa na ondoka ilikupata fursa kubwa zaidi.

Kuna msemo mmoja unasema A good dancer knows when to leave the stage.Yaani mchezaji mzuri anajua ni muda gani wa kuondoka jukwaani.Hapa niseme tu kwamba kuna watu hawana kiasi katika mambo,utashangaa mtu anakalia kuchati kwenye mitandao ya kijamii kuanzia asubuhi hadi jioni tena bila ukomo na hakuna anachopata zaidi ya umbea na kupoteza muda.Ifahamike kuwa kutumia mitandao ya kijamii siyo vibaya kikubwa ni kuwa na kiasi katika kutumia na itumike kwa manufaa na si vinginevyo,pia kuwa na kiasi katika kuzungumza.

Kuwa na kiasi na zaidi fanyia kazi ndoto yako wakati huu kabla exit time yako haijafika,pambana kila kitu kinawezekana.Acha kufuata mikumbo ya watu wengine,kuwa wewe jifunze kwa watu lakini usiwaige.Kila kitu hakuna kisichowezekana tambua majira na nyakati katika maisha yako itakusaidia sana kujua nini ufanye na wakati gani. Hakika itakuwa ni hatua kubwa sana katika kuifanyia kazi ndoto yako.

 

rafiki! ni matumaini yangu kuwa umejifunza kitu.

na kama unachangamoto katika hili pengine namna gani ya kuondokana na adha hii wasiliana na mimi moja kwa moja kupitia mawasiliano hapo chini naamini utasaidika.

GeT tO ThE nExT lEvEl!

Makala hii imeandaliwa na kuandikwa na MIGONGO ELIAS Mshauri & Mwalimu Wa Saikolojia,Uchumi na Maisha.Mwanzilishi na Mwendeshaji wa Mtandao wa addvaluetz.Karibu sana ujiongezee thamani yako. 

Kwa mawasiliano;

Whatsapp & Sim >>+255767653697 /+255783327456

Email>> eliasmigongo120@gmail.com.

Facebook>> MIGONGO ELIAS.

LinkedIn>>Migongoe. 

Pinterest>>eliasmigongo.

Kama umejifunza kitu,niachie maoni yako nitafurahi kujifunza pamoja nawe. 

Popular posts from this blog

GHARAMA 5 ZA KUUFIKIA UKUU UNAOUTAKA.

USIKUBALI KUAJIRIWA KABLA HUJASOMA HAPA.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.