MAAJABU YA AKIBA

Image
MAAJABU YA AKIBA Akiba (saving) ni kiasi cha fedha au rasilimali ambacho kimewekwa kwa matumizi ya baadaye, hata sasa kingeweza kutumika lakini umuhimu wake kwa kutumika baadaye ni mkubwa kuliko matumizi yake ya sasa. Hata katika biblia ``Mwanzo 41:35-36`` kama umewahi soma utaona Farao baada ya kutafsiriwa ndoto yake na kufahamu kuwa, imempasa kuweka akiba alilifanya hilo kwa uharaka ili kuhakikisha linaendelea vizuri ndio akamweka Yusufu kama msimamizi wa hili. Farao aliona kabisa kuwa nidhamu yake ya kujiwekea akiba haipo sawa hivo alihitaji msaidizi wa kumsaidia kama yeye alivyokuwa ndivyo tulivyo baadhi yetu siku za leo hatuwezi kujiwekea akiba ya vile tulivyo navyo. yaani huwa tunapenda kusema kesho itajisumbukia yenyewe,  Hata hivyo tangu zamani hata leo mataifa mbalimbali yamekuwa yakijiwekea akiba kwa manufaa na matumizi ya baadaye. Ukiangalia nabii Samweli alikuwa akijiwekea akiba na aliitoa pale Sauli alipomtembelea wakaila ile akiba ya chakula. Ni muhimu kujiw...

CHANGAMOTO KATIKA MAISHA

 

             CHANGAMOTO KATIKA MAISHA. 

Changamoto inaweza kuwa na maana nyingi, lakini wacha tukubaliane kuwa changamoto ni ugumu au vizuizi anavyokutana navyo mtu katika kuyaendea yale aliyoyakusudia. Yaani, malengo na ndoto zako. 

Wakati mwingine changamoto ni jaribu katika eneo fulani la maisha ya mtu husika. 

Katika hili nimegundua kuwa changamoto haiji kwa lengo la kukuharibu, kukukomoa, kukurudisha nyuma, au kukufanya ushindwe kabisa. 

Lakini, changamoto ipo kwa lengo la kukupima na kukuthibitisha kwamba umekizi vigezo vya kuwa au kuvuka katika hatua fulani ya maisha uliyopo na kwenda hatua nyingine.

Wakati mwingine ugumu au changamoto ni kipimo cha kuufikia ushindi. 

Ukweli ni kwamba, huwezi kuwa mshindi pasipo kushindana, kama ndivyo hivyo, sasa katika mashindano hayo utakutana na ugumu fulani ambao ndiyo changamoto zenyewe.

Kadiri unavyotatua na kushinda changamoto nyingi na kubwa ndivyo unavyokuwa bingwa na mshindi katika eneo hilo. 

Wakati mwingine, changamoto inalenga sana katika kutuimarisha. 

Changamoto ni kama moto kwa dhahabu, dhahabu huimarika na kuwa imara zaidi pindi inapopita katika moto. Hivyo, lengo la changamoto kwa mtu ni kumuimarisha mtu huyo. 

Ndiyo maana mtu anapokutana na jaribu au changamoto akapambana na kuishinda hatakuwa kama alivyoingia kwenye changamoto hii, hapo utakutana na mtu ameongeza ujasiri na kujiamini zaidi. 

Moja ya faida ya changamoto ni kwamba inatupa uzoefu katika maisha yetu na uzuri wa uzoefu ni kwamba unatupunguzia makosa. 

Hivyo kumbe changamoto na ugumu unaopitia ni sehemu ya maisha na ipo kwa mema na si kwa lengo la kukukomoa kama wewe unavyofikiri.

Hebu chukulia katika maisha kusingekuwa na ugumu wowote yaani, kila kitu ukikitaka unakipata wakati huo huo, kwa namna ileile kwa kiwango kilekile pasipo shida na ugumu wowote, unadhani maisha yangekuwaje?

 Pamoja na kwamba Maisha yangekuwa mepesi sana, sidhani kama tungekuwa wabunifu, watu wa bidii, wavumilivu n. k

Siku za nyuma nilikuwa na mtazamo ambao kiuhalisia siyo sahihi kabisa. 

Nilikuwa najua kuwa, kunawatu fulani fulani hivi hawapitii kabisa changamoto na ugumu katika maisha yao. Kumbe  ulikuwa ni mtazamo ambao hata sio sahihi. 

Ndugu, tambua kuwa hakuna mtu hata mmoja asiyekutana na ugumu katika eneo fulani la maisha yake

Pia ni muhimu kufahamu kuwa Kila mtu ana ugumu na matatizo yake ambayo yanaweza yasifanane kabisa na matatizo yako.

Ukiishi na mtazamo huo itakuwa ni mwanzo wa kukata tamaa (give up), msongo wa mawazo (stress), kujidharau na kuona hufai pengine huna akili kabisa.

Ukifahamu malengo na faida za changamoto huna haja ya kulalamika na kuwanung'unikia watu wengine wakati mwingine hadi kumlaumu Mungu mwenyewe. 

Niandike kukwambia kuwa, changamoto zipo kwa watu wote na zipo kila hatua ya maisha unayoifikia. 

Na kwa wale wanao mwamini Mungu tufahamu kuwa kumwamini Mungu haimaanishi kuwa hutakutana na ugumu katika maisha yako. Hii inamaana kuwa, pamoja na ugumu utakao kutana nao Mungu atatupa uwezo wa kukabilina nazo. 

Pia elewa kuwa matatizo yapo kwa watu wote na si kwa baadhi ya watu kama unavyo dhani. 

Kila ukimaliza kutatuza tatizo kwenye maisha yako, uwezo wa kukabilina na matatizo huongezeka hivyo unapewa matatizo makubwa zaidi ya mwanzo.

Hapa ndipo utagundua kuwa, kila ukivuka changamoto fulani unakutana na changamoto nyingine ambayo hukutegemea kabisa, tena wakati mwingine ni kubwa kuliko ile ya mwanzo. Na sababu yake ni kwamba, uwezo wako wa kutatua matatizo umepanda viwango na wewe unapewa changamoto za viwango.

 Ndiyo maana maandiko matakatifu yanasema

"Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili (1 Wakorintho 10:13)".

Hapa tunapata funzo ya kwamba Kila changamoto inayokuja mbele yako, tambua kabisa kuwa unaweza na ipo ndani ya uwezo wako, kwababu tumeona kuwa Kila mtu anapewa changamoto kulingana na uwezo wake. Hapa ndipo atakapo ikabili ataishinda na ikionekana ni ngumu Mungu anasema atafanya mlango wa kutokea.

Hivyo hata kama unaona ugumu unaopitia umekuwa mkubwa sana tambua kuwa upo na uwezo nao na kinachotakiwa ni kupambana mwanzo mwisho hata utakapo uona ukuu. 

Utakutana na changamoto katika biashara, katika ndoa, kwenye kilimo, kanisani, shuleni, kwenye siasa, kwenye uchumi, michezo na sehemu nyingine kibao. 

Tambua kuwa pamoja na changamoto hizo, unao uwezo wa kupambana nazo na kuzishinda kabisa. 

Watu waliofanikiwa si kwamba hawakutani na changamoto laah! utagundua wanapitia changamoto tena kubwa tu! Lakini wanapambana nazo kimaso maso hadi kuufikia  ukuu wao.

Na wewe nikuambie, kuna ukuu fulani hautaufikia hadi utakapo ivuka changamoto hiyo, pambana , usikate tamaa, vumilia hata utakapo ivuka na ukuu unaoutaka utaufikia.

Changamoto yako ni yako mwenyewe pambana nayo hadi uishinde, usidhani kuna mtu atakuja from no where aje akupambanie. 

KUNA MAHALI HAUTAFIKA HADI UTAKAPO IVUKA HIYO CHANGAMOTO YAKO.

Ndugu naweza kuzungumza mengi sana katika hili, lakini, wacha kwa leo nisema kwamba, changamoto ni mtaji, ni njia ya kuuendea ukuu wako. 

Na ugumu wa maisha ni kipimo cha akili.

 "Ndugu zangu, hesabuni ya kuwa ni furaha tupu, mkiangukia katika majaribu mbalimbali;(Yakobo 1:2)". 

Kama wewe ni mtu wa kutamani mafanikio makubwa huku ni mtu wa kuogopa changamoto hautafikia mafanikio hayo badala yake utaishia kuyatamani tu, kusingizia mikosi , laana, wachawi, na kujiita huna bahati. 

Hakuna namna ya kuufikia ukuu huo pasipo kupambana na kuzishinda changamoto zako. 

Rafiki, ni matumaini yangu kuwa umejifunza kitu.

Na kama unachangamoto katika hili pengine namna gani ya kuondokana na changamoto yako, sasa waweza kuwasiliana na mimi moja kwa moja kupitia mawasiliano hapo chini naamini utasaidika.

GeT tO ThE nExT lEvEl!

Makala hii, imeandaliwa na kuandikwa na MIGONGO ELIAS Mshauri & Mwalimu wa Saikolojia, uchumi, maendeleo binafsi na Maisha

Mwanzilishi na Mwendeshaji wa Mtandao wa addvaluenetwork

Karibu sana ujiongezee thamani yako. 

Kwa mawasiliano;

Whatsapp & Sim >>+255767653697 /+255783327456

Email>> eliasmigongo120@gmail.com.

Facebook>> MIGONGO ELIAS.

Fb page>>> add value network.

Kama umejifunza kitu, niachie maoni yako nitafurahi kujifunza pamoja nawe. 

Comments (6)

Loading... Logging you in...
  • Logged in as
Ayusto Busanda's avatar

Ayusto Busanda · 98 weeks ago

Hiyo ni kweli bado nazidi kupata madina kutoka kwako mwl.migongo Mungu akutumie zaidi
1 reply · active 98 weeks ago
Amen amen Ayusto Busanda barikiwa sana
Anna Isack's avatar

Anna Isack · 76 weeks ago

Asantee mtumishi Kwa kunitia nguvu katika changamoto yangu ninayo pitia hakika Mungu ni mwaminifu Ubarikiwe sana
1 reply · active 76 weeks ago
Amen amen Ubarikiwe piaa ndugu
Ubarikiwe saana mwl kwa Somo zuri.
1 reply · active 76 weeks ago
Amen amen nashukuru ndugu

Post a new comment

Comments by

Popular posts from this blog

NJIA 7 ZA KUOSHA UBONGO WAKO.

VITU 9 MUHIMU KWA MTU YEYOTE KUJIFUNZA KWENYE MAHAFALI.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.