MAAJABU YA AKIBA

Image
MAAJABU YA AKIBA Akiba (saving) ni kiasi cha fedha au rasilimali ambacho kimewekwa kwa matumizi ya baadaye, hata sasa kingeweza kutumika lakini umuhimu wake kwa kutumika baadaye ni mkubwa kuliko matumizi yake ya sasa. Hata katika biblia ``Mwanzo 41:35-36`` kama umewahi soma utaona Farao baada ya kutafsiriwa ndoto yake na kufahamu kuwa, imempasa kuweka akiba alilifanya hilo kwa uharaka ili kuhakikisha linaendelea vizuri ndio akamweka Yusufu kama msimamizi wa hili. Farao aliona kabisa kuwa nidhamu yake ya kujiwekea akiba haipo sawa hivo alihitaji msaidizi wa kumsaidia kama yeye alivyokuwa ndivyo tulivyo baadhi yetu siku za leo hatuwezi kujiwekea akiba ya vile tulivyo navyo. yaani huwa tunapenda kusema kesho itajisumbukia yenyewe,  Hata hivyo tangu zamani hata leo mataifa mbalimbali yamekuwa yakijiwekea akiba kwa manufaa na matumizi ya baadaye. Ukiangalia nabii Samweli alikuwa akijiwekea akiba na aliitoa pale Sauli alipomtembelea wakaila ile akiba ya chakula. Ni muhimu kujiw...

HATUA 4 ZA KUSEMA HAPANA KWA HESHIMA.

 

HATUA 4 ZA KUSEMA HAPANA KWA HESHIMA.

Asilimia kubwa ya watu duniani, wanakumbwa na changamoto ya kushindwa kusema hapana kwa ombi waliloombwa kufanya. 

Hii inatokea mara nyingi wakati mwingine wanapohitajika kuwafanyia hivyo wapendwa wao, rafiki zao, majirani zao, wazazi, ndugu na jamaa wa karibu. 

Pia inatokea pale unapohitajika kufanya hivyo huku huna uwezo kabisa wa kufanya au kutoa msaada huo. 

Lakini kwa kuogopa kuwaumiza, kuwavunja moyo na kupoteza heshima, watu wengi hujikuta wakisema ndiyo hata sehemu walipotamani kusema hapana. 

Hii husababisha mtu kuishi maisha ya watu wengine na yenye maumivu makali sana.

 Kama unachangamoto hii usiogope, kwani hauko pekee yako ni watu wengi sana duniani wanapitia changamoto hii. 

Lakini habari njema ni kwamba hapa nimekuandalia hatua nne za kusema hapana bila kuogopa, bila kuvunja heshima yako au kuharibu mahusiano yako na watu wengine, 

Soma hadi mwisho nina imani utasaidika;

HATUA YA KWANZA:  

ONYESHA KUTHAMINI (SHOW APPRICIATION).

Kama unataka kukataa ombi la watu ambalo lipo nje ya uwezo wako, bila kuvunja mahusiano yako na watu wengine. Basi ni muhimu kufuata hatua hii ya kwanza ya  kushukuru na kuthamini nafasi hiyo ya kuombwa msaada kwani si kila mtu atapata nafasi hiyo. 

Kwani ukweli ni kwamba hadi mtu anapokuja kukuomba msaada anakuwa amekuthamini na kukuamini  sana hadi kukutafuta umsaidie kutatua changamoto hiyo. 

Hivyo ni muhimu kulitambua hilo na kumshukuru sana kwa kukuamini. 

Hapo ni muhimu kusikiliza kwa makini, kuuvaa uhusika, ikiwezekana uliza maswali na onyesha kuguswa na changamoto hiyo.

 Mfano mtu anaweza akaja anataka umkopeshe  100,000/= ili akaongezee mtaji, wakati huo na wewe huna hela ya kutosha kumsaidia. 

Unaweza kumwambia hivi,  "Hongera sana kwa namna ambavyo unapambana kukuza na kuendesha biashara yako. Lakini pia, nashukuru sana kwa kutambua kuwa ninaweza kukusaidia katika hili...".

Soma tena hapo.

Wacha tuende hatua ya pili sasa.

HATUA YA PILI: 

SEMA HAPANA YA KUELEWEKA UTOE NA SABABU YAKE.

Kutoka sehemu ya kwanza ambapo umesikiliza na umefahamu shida ya mtu huyo kwa undani lakini pia umeonyesha kushukuru na kuthamini nafasi hiyo ya kuaminiwa. 

Sasa hii ni hatua ya muhimu sana ambayo inawashinda wengi, nayo ni kusema hapana lakini siyo hapana tu, bali eleza na sababu yake. 

Ukirejea kwenye mfano wetu hapo juu wa mkopo wa 100,000/= ambayo huna.

Mwambie mtu ukweli mapema kabla hamjafika mbali, na ukweli wenye ni hapana.

Kusema hapana ni ngumu kidogo kuisema sasa goja tuiseme hapana kwa heshima kutokana na mfano huo. 

Unaweza kusema hivi, nashukuru sana kwa kutambua kuwa nina weza kukusaidia katika hili.

"Lakini nasikitika kwamba sitaweza kukusaidia katika hili. Kwa kingereza ndo nzuri zaidi (am sorry that I won't be abble to do so)". 

Na usiishie kusema hivyo tu hatakuelewa na utamvunja moyo kweli, hapo, lazima utoe na sababu kwanini huwezi kumsaidia. 

Sababu ya hapo juu unaweza kusema staweza kukusaidia katika hili kwasababu jana nimefanya mahemezi lakini pia nimelipia ada ya watoto shuleni, nimetumia pesa nyingi sana (usidanganye weka sababu yako hapa), na hii kupelekea mfuko wangu kuyumba, hivyo itakuwa ngumu kidogo kukusaidia... 

Hallo sijui kama unanielewa? 

Kama unanielewa punga mkono🖐️ 

Okey sasa tende hatua ya tatu tukaone sote.

HATAUA YA TATU: 

TOA OFA YA KUKANUSHA OMBI HILO.

Mama mmoja ambaye ni mama mlezi kwangu aliwahi kuniambia, "wakati mwingine msaada siyo lazima upewe pesa tu!  Kama watu wengi walivyo kariri".

Tafadhali rudia kusoma tena uelewe.

Sasa na hatua hii ya tatu isiishie kusema hapana na sababu yako tu. 

Watu wengine wana roho ndogo wanaweza kukuelewa vibaya na wakavunjika moyo. Hivyo basi, badala yake unaweza kuwepatia ofa ya kitu unacho kiweza kuwasidia kwa wakati huo. Tafadhali Soma tena.

Yaani, nazungumzia unaweza kutoa msaada mbadala ya pesa, hii inawezakuwa ushauri, muda, kiasi cha fedha ambacho unaona utakimudu na mengine kibao. 

Hebu turudi kwenye mfano wetu, hapa unaweza kumpa ofa ya kumshauri, au wakati mwingine kumwonyesha sehemu wanayotoa mkopo wa riba nafuu, au una weza kumwelekeza sehemu wanako chukua bidhaa kwa bei nafuu sana ambapo anaweza kujibana kwa mtaji huo huo alio nao na kudunduliza kidogo kidogo hatimae atakuwa na kiasi cha kutosha kama anavyotaka yeye.

Si unajua hata mbuyu ulianza kama mchicha ee!

HATUA YA NNE: 

PATA MREJESHO NA MJULIE HALI.

Daada ya kupitia hatua hizo zote tatu za kusema hapana sasa, ili kuimarisha mahusiano na urafiki wenu usiishi hapo tu, endelea kuwasiliana nae na kuuliza hali na mwenendo wa biashara yake. 

Hapo anaweza kukupa changamoto anazokumbana nazo, endelea kumshauri na kumpa mwelekeo zaidi ili kukuza na kuendeleza biashara na maendeleo yake binafisi. 

Hii, itaonyesha kuwa kweli uliguswa na ombi lake.

Na hii itaongeza heshima na kukuamini zaidi. 

Niseme tu kuwa, watu wengi wameingia kwenye migogoro, madeni, kesi, kuvunja heshima na hata kuvunja uhusiano wao na watu wengine  kwasababu ya kushindwa kusema hapana. 

Kama utatumia njia hizo hapo juu tatizo hili litabaki historia kwako. 

Nb: usiseme ndiyo au hapana ili kumridhizisha mtu, sema hivyo kwasababu unaweza na ipo ndani ya uwezo wako.

Soma tena hapo juu.

Na ukishindwa kufanya hivyo utaishi maisha ya watu wengine na ya kitumwa kabisa . 

kuna msemo mmoja naupenda sana lakini ni wa kingereza ila usijali tutautafisiri nao ni huu 

 “If you have nothing to say, say nothing”. Yaani, kama huna cha kusema, kaa kimya.

Lakini pia ni muhimu kutambua kuwa kunasehemu za kusema hapana na sehemu za kusema ndiyo tusichanganye mambo hapo. 

Na tatizo huanzia wakati wa kusema hapana mtu anasema ndiyo  na penye ndiyo mtu anasema hapana. 

Huu nao sijui ni ukosefu wa nini!

Jipongeze kwa kusoma hadi mwisho.

Rafiki, ni matumaini yangu kuwa umejifunza kitu.

Na kama unachangamoto katika hili pengine namna gani ya kuondokana na adha hii, sasa waweza kuwasiliana na mimi moja kwa moja kupitia mawasiliano hapo chini naamini utasaidika.

GeT tO ThE nExT lEvEl!

Makala hii, imeandaliwa na kuandikwa na MIGONGO ELIAS Mshauri & Mwalimu Wa Saikolojia, Uchumi na Maisha.

 Mwanzilishi na Mwendeshaji wa Mtandao wa addvaluenetwork

Karibu sana ujiongezee thamani yako. 

Kwa mawasiliano;

Whatsapp & Sim >> +255767653697.

Email>> eliasmigongo120@gmail.com.

Facebook>> MIGONGO ELIAS // Add Value Network.

Kama umejifunza kitu fanya yafuatayo;

Moja: washirikishe na wengine kwa kuwatumia somo hili.

Mbili: follow, like na comment kwenye Facebook page zetu.

Tatu: Save namba yangu, Kisha nitumie jina lako WhatsApp nami nisave, ili tuwe marafiki na tujifunze zaidi.

  


 

Comments (8)

Loading... Logging you in...
  • Logged in as
Ayusto Busanda's avatar

Ayusto Busanda · 97 weeks ago

Ni sawa kabisa Mwl zidi kuinuliwa zaidi katika huduma hii
1 reply · active 97 weeks ago
Amen amen Ayusto Busanda.
Thank you sir,It's powerful messages
1 reply · active 97 weeks ago
Thank you so much Mr Eliud
Asanteh kwa kuniongezea maarifa juu ya namna ya kutumia maneno haya ndiyo na Hapana. Mungu azidi kukutumia, Barikiwa saana.
1 reply · active 96 weeks ago
Elias Migongo's avatar

Elias Migongo · 96 weeks ago

Ahsante nashukuru Cheyo g.
What a message. Hili ni tatizo kwa watu wengi na inawatesa mamia kwa maelfu ya watu. Katika jamii zetu kwa utamaduni wa Kitanzania tunasumbuliwa na utamaduni wa aibu yaani shame culture ambao tunataka tuwapendeze watu kwa kila jambo kusema hapana inakuwa ni ngumu na katika hili wengine hata wanaenda mbali kukopa kwaajili ya kuwasaidia wengine na mwishowe wanaangua kwenye madeni. Msaada wako sio lazima kwasasa kama huna uwezo sema hapana ili kujiondolea mzigo usio wa lazima then kwa siku zijazo waweza kusaidia pale utakapokuwa na uwezo.

Joel Nanauka anasema: unaweza tu kumimina maji kwenye kikombe kilichojaa; kuna watu wanataka kumimina maji kwenye kikombe kitupu mwisho wa siku utaishia kushindwa kujisaidia mwenyewe na wale wanaokuzunguka kwa muda sahihi watakao hitaji msaada wako.
1 reply · active 44 weeks ago
Nimejifunza Sana ahsante nashukuru ndugu

Post a new comment

Comments by

Popular posts from this blog

NJIA 7 ZA KUOSHA UBONGO WAKO.

VITU 9 MUHIMU KWA MTU YEYOTE KUJIFUNZA KWENYE MAHAFALI.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.