MAAJABU YA AKIBA

Image
MAAJABU YA AKIBA Akiba (saving) ni kiasi cha fedha au rasilimali ambacho kimewekwa kwa matumizi ya baadaye, hata sasa kingeweza kutumika lakini umuhimu wake kwa kutumika baadaye ni mkubwa kuliko matumizi yake ya sasa. Hata katika biblia ``Mwanzo 41:35-36`` kama umewahi soma utaona Farao baada ya kutafsiriwa ndoto yake na kufahamu kuwa, imempasa kuweka akiba alilifanya hilo kwa uharaka ili kuhakikisha linaendelea vizuri ndio akamweka Yusufu kama msimamizi wa hili. Farao aliona kabisa kuwa nidhamu yake ya kujiwekea akiba haipo sawa hivo alihitaji msaidizi wa kumsaidia kama yeye alivyokuwa ndivyo tulivyo baadhi yetu siku za leo hatuwezi kujiwekea akiba ya vile tulivyo navyo. yaani huwa tunapenda kusema kesho itajisumbukia yenyewe,  Hata hivyo tangu zamani hata leo mataifa mbalimbali yamekuwa yakijiwekea akiba kwa manufaa na matumizi ya baadaye. Ukiangalia nabii Samweli alikuwa akijiwekea akiba na aliitoa pale Sauli alipomtembelea wakaila ile akiba ya chakula. Ni muhimu kujiw...

JAMBO HILI HALITAKUACHA SALAMA.

 

KITU HILI HAKITAKUACHA SALAMA.

Mtu mmoja alikuwa analalamika sana huku akidai kuwa, amejifunza vitu sana ikiwemo kulima, kushona nguo, amesoma sana kompyuta, kufanya biashara, kama ni vitabu amesoma sana. Kimsingi alidai kuwa anajua karibia kila kitu. Lakini alichokuwa analaumu kwamba haoni badiliko lolote kabisa katika maisha yake, licha  ya kujifunza vitu na maarifa kama yote. Nilipo muuliza, kwenye kompyuta anajua kitu gani? Akasema anafahamu kompyuta yote na amejifunza miaka miwili iliyopita na notisi aliandika zote sema hakumbuki daftali alipoliweka, lakini akituliza akili atalipata mara moja. Nikamuuliza nikileta kompyuta hapa unipangie kazi yangu utaweza? Akasema, hivyo vyote nilisha visoma na niliviandika tena vipo kwenye lile daftali, sema kompyuta mi sijawahi kutumia lakini nikiangalia kwenye lile daftali naweza afu mbona ni simpo tu. 

Nikagundua kuwa mtu huyo alikuwa ametumia muda mwingi na gharama kubwa sana katika kujifunza vitu vingi sana. Alikuwa ameandia notisi na hatua zote muhimu ili kuvifanikisha vitu hivyo. Ajabu ni kwamba  ingawa alikuwa   amejifunza vitu vingi, lakini hakuwahi kuvifanyia kazi na vingine hata hakuvifahamu kabisa. Mfano alikuwa amejifunza kilimo cha nyanya mtandaoni, lakini hakuwahi kulima hata siku moja, pia alikuwa amejifunza kutengeneza sabuni ya mche, unga na maji lakini hakuwahi kutengeneza hata sabuni moja, alijifunza sheria za fedha na namna ya kuepukana na madeni kwenye kitabu cha Tajiri mkubwa wa babeli, lakini hakuwahi kuzingatia na kufanyia kazi hata kimojawapo japo alikuwa anazifahamu, pia alikuwa amejifunza kompyuta na matumizi ya kompyuta lakini hakuwahi kutumia kompyuta, na vitu vingine kedekede ambavyo alinitajia.

Ikumbukwe kwamba si kwamba vitu hivi alikuwa amevisahau vyote hapana, vingi alikuwa anavikumbuka kabisa lakini pamoja na kuvikumbuka kwake bado alikuwa anaona maisha yake  yako vilevile hayabadiliki kabisa. Yaani, kama ni madeni yalizidi kuongezeka, kama kudharaulika ndo usiseme, kukosa pesa ndo kabisa n.k.

Mtu huyo nilimuuliza kwamba unafahamu sababu kwanini bado maisha yako hayabadailiki ingawaje unamaarifa na unafahamu vitu vingi? Akasema bado hajafahamu shida ni nini? Nikamwambia usipolifahamu tatizo huwezi kulitatua tatizo, vinginevyo itakuwa ni chanzo cha matatizo mengine. Akaomba nimusaidie sana katika kulifahamu tatizo lake kwani nilikuwa namfahamu vizuri. Hapo ndipo nilipoamua kumsaidia na kumwambia tatizo lake liko wapi, na tatizo lake lilikuwa ni hili hapa.

Kutokufanyia  mazoezi kitu alicho jifunza yaani nasema, kutokufanyia kazi au utekelezaji maarifa aliyokuwa amejifunza na kuyafahamu.  Aidha, kwa kuambiawa, kujifunza au kwa kufundishwa. Kitu hiki hakikumwacha salama kabisa. Nasema hivi kutokufanyia kazi maarifa aliyo nayo hiki kitu hakikumwacha salama kabisa, kwani alibaki na matatizo yake hata kama alikuwa na maarifa kama yote. Nilimshauri na kumwambia maisha yake yatabadailika endepo ataamua kufanyia kazi , kutekeleza na kufanyia mazoezi ya mara kwa mara katika kila atakacho jifunza, ambacho kinalenga kuboresha maisha yake, fanyia kazi tena kwa bidii. 

Namshukuru Mungu kwamba alikuwa mwelewa na aliamua kufanya mazoezi ya mara kwa mara katika juzi zote alizokuwa amejifunza na atakaokuwa anajifunza, na kuanzia hapo maisha yake yalianza kubadilika kabisa na Hadi Sasa amekuwa mtu mwenye mchango mkubwa sana kwa watu waliomzunguka na jamii yake kwa ujumla, na hadi sasa ni mtu ambaye anafanya vizuri na kuna mengi ya kujifunza kutoka kwake.

Hivyo ndugu kitendo cha wewe kutofanyia mazoezi vitu ambavyo unajifunza kwaajili ya maandeleo na maisha yako kwa ujumla, kitu hiki hakita kuacha salama.

Kutochukua hatua ya kufanyia kazi au utekelezaji wa  maarifa unayo jifunza kila siku kwa manufaa yako mwenyewe hiki kitu hakitakuacha salama.

Katika hili ni muhimu kufahamu kuwa kusoma na kuyafahamu maarifa ni jambo moja, na kuchukua hatua,utekelezaji au kufanyia kazi maarifa hayo ni jambo lingine tena la tofauti kabisa. Yaani, kusoma vitabu pekee hakutoshi, kujifunza pekee hakutoshi na kufahamu vitu vingi pekee yake hakuwezi kukufanikisha wala kukufikisha unakotaka. 

Kufanya hivyo ni vizuri sana tena ni hatua ya kupongezwa, pengine hatakupewa zawadi kabisa lakini kunahatua muhimu ya pili ambayo unahitaji kuipiga baada ya kuvifahamu vitu vyote hivyo, nayo ni utekelezaji (kufanyia kazi). Hapo unahitaji kufanyia kazi kitu utakachojifunza na kuona kuwa kina manufaa katika maisha yako vinginevyo mabadiliko utayasikia tu.

Ulishawahi kujiuliza ingekuwaje wachezaji wa mpira wangekuwa wanasomeshwa mpira darasani wanaacha hivyohivyo bila kufanyia mazoezi ya kile walichojifunza? Vipi kuhusu wakulima wangekuwa wanasoma kilimo darasani pekee yake bila kwenda kufanyia mazoezi  mafunzo hayo? Au ulisha wahi kujiuliza kwanini baadhi ya watu pamoja na kufundishwa uzalendo, maadili na dini kila siku lakini bado dhambi na maasi vinazidi kuongezeka ?

Hapo ndipo utakuja kujua kumbe kujifunza pekee yake hakujitoshelezi, kujua vitu vingi pekee yake hakujitoshelezi hapo unahitaji hatua moja mbele zaidi, ambayo ni  kufanyia kazi tena kwa bidii  kile ambacho unakifahamu au umejifunza. Umejifunza kulima vitunguu nenda kalime, umejifunza kutengeneza sabuni nenda katengeneze, umejifunza biashara nenda kafanye, umejifunza uwekezaji nenda kawekeze, umejifunza uandishi nenda kaandike. Yaani, nasema nenda kafanyie mazoezi huo ujuzi wako, hiyo ndoto yako, hicho kipaji chako vinginevyo kitu hiki  hakitakuacha salama.

Usiwe kama wale wengine ambao wakifahamu kitu ndo imeenda hiyo na wengine hawataki hata kufanyia kazi na mazoezi ya kile walichojifunza huku wakitegemea maisha yao kuna siku tu yatabadilika yenyewe bila kufanyia kazi.

Mwingine utakuta anakipaji kizuri kweli lakini hataki kukinoa na kukifanyia mazoezi akisema eti yeye anakipaji kikubwa, ndugu tambua kuwa kipaji chako hata kiwe kikubwa kiasi gani kama hukinoi na kukifanyia kazi utabaki kuwa mtu wa kawaida sana, hebu jifunze kwa watu wenye vipaji vyao kama akina Diamond platinum, Messi, Ronaldo, Mbwana Samata na wengine kibao. Watu hawa pamoja na kuwa na vipaji hawajaacha kufanyia kazi juzi zao na vipaji vyao katika kufanikisha na kufikia ndoto zao. Na wewe kama unatabia ya kutafuta maarifa, kujifunza kwa bidii lakini hufanyii kazi kile unachojifunza yaani, unalala tu huna muda wa kufanya mazoezi maarifa hayo. Nikwambie tu ukweli kuwa jambo hili halitakuacha salama.

Rafiki! ni matumaini yangu kuwa umejifunza kitu.

na kama unachangamoto katika hili pengine namna gani ya kuondokana na adha hii wasiliana na mimi moja kwa moja kupitia mawasiliano hapo chini naamini utasaidika.

GeT tO ThE nExT lEvEl!

Makala hii imeandaliwa na kuandikwa na MIGONGO ELIAS Mshauri & Mwalimu Wa Saikolojia, Uchumi na Maisha. Mwanzilishi na Mwendeshaji wa Mtandao wa addvaluetz. Karibu sana ujiongezee thamani yako. 

Kwa mawasiliano;

Whatsapp & Sim >>+255767653697 /+255783327456

Email>> eliasmigongo120@gmail.com.

Facebook>> MIGONGO ELIAS.

LinkedIn>>Migongoe. 

Pinterest>>eliasmigongo.

Kama umejifunza kitu, niachie maoni yako nitafurahi kujifunza pamoja nawe. 

 

 

Comments (8)

Loading... Logging you in...
  • Logged in as
Nimejifunza sana mwalimu Eliasi mm ni moja kati ya watu waliokuwa hawaoni faida ya vtu vingi walivyojifunza lkn sasa baada ya kuchukua uamuz wa kutendea kaz maarifa yangu nikaanza kuona mabadiliko makubwa katika maisha yangu
1 reply · active 101 weeks ago
Ahsante sana Nuru kwa ushuhuda wako.
Binafsi nikushukuru sana ni somo zuri mwenyewe naona matokeo
1 reply · active 100 weeks ago
Ahsante sana Ayusto
Agripina Mghamba's avatar

Agripina Mghamba · 79 weeks ago

Hili Ni somo zuri mno.
Nimejifunza mengi.
Mungu AKUBARIKI MNOOOOO 🙌
2 replies · active 79 weeks ago
Agripina Mghamba's avatar

Agripina Mghamba · 79 weeks ago

Kutendea kazi unachojifunza🧏🧏🧏🧏
Sio kuishia tuu kujaza notebook
Ahsante nashukuru Sana Agripina
Wooow, umenena point hapo....asee

Post a new comment

Comments by

Popular posts from this blog

NJIA 7 ZA KUOSHA UBONGO WAKO.

VITU 9 MUHIMU KWA MTU YEYOTE KUJIFUNZA KWENYE MAHAFALI.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.