HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 26.

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 26. Ilipoishia.......... Alipomgeuza tu alishangaa kuona sura ya yule binti ni ya mbuzi. Aliogopa na kudondoka chini kwa kelele kuu alilia 'maaamaaaaaaa!!!!" Alijiokotaokota huku akiangukaanguka mpaka kwenye gari yake. Alipanda ndani ya gari na kuwasha gari. Alikimbiza gari mpaka akafika karibu na geti la nyumba ya Elvine, lakini kabla hajafika getini alishangaa kuona anaguswa mabegani ndani ya gari lake. Alitoa macho kwa uoga na mshtuko mkubwa mpaka akakosea njia na kwenda kugonga mti... Kusoma sehemu ya 25 bonyeza hapa. Sasa inaendelea......, Aligonga mti kwa nguvu mpaka naye akajipigiza kichwa kwenye usukani wa gari na gari ikaharibika sana upande wa mbele, alipona kwa neema tu kwa namna gari ilivyokuwa mwendo kasi angeweza hata kupoteza maisha lakini haikuwa hivyo. Alijikaza na kushuka kwenye gari akakimbia kuelekea kwenye nyumba ya Elvine,  njiani alikumbwa na kimbunga cha ajabu sana. Baada ya kile kimbunga kumpitia na kumzingazinga kwa muda

SABABU 7 ZA HOFU YA KUZUNGUMZA MBELE YA WATU (REASONS FOR FEAR OF PUBLIC SPEAKING).

 

SABABU ZA HOFU YA KUZUNGUMZA MBELE YA WATU (REASONS FOR FEAR   OF PUBLIC SPEAKING).

Nakumbuka nilipokuwa sekondari kidato cha kwanza, mara nyingi nilipokuwa nikipangwa kuzungumza hotuba ya asubuhi (Morning speech). Nilikuwa nahisi kuchanganyikiwa, kuugua, kukosa utulivu, kutokwenda shule  na wakati mwingine nilikuwa nawaza hadi kuacha shule. Yaani, nilikuwa na hofu isiyokuwa ya kawaida lilipokuja suala la kujieleza na kuzunguza mbele ya kadamnasi. Lakini Namshukuru Mungu kwakuwa alinikutanisha na waalimu pamoja na watu sahihi wakanisaidia nikawa nafanya vyema katika eneo hilo.

Katika mizunguko yangu hadi sasa nimekuja kugundua kuwa siyo mimi tu niliyekuwa na tatizo hilo, kumbe ni watu wengi sana wakubwa kwa wadogo, waume kwa wake  tena karibia watu wote duniani. Kwani hata tafiti zinaonyesha kuwa asilimia(75%) ya watu duniani wanasumbuliwa na hofu hii . Hofu hii ni moja ya hofu zinazo ogopeka na kutesa watu wengi sana duniani. Hapo ndipo utakuja kushangaa mtu alikuwa sawa kabisa kabla ya kupita mbele ya  watu lakini baada tu ya kupita ili kuzungumza  mbele yao, utashangaa sauti inabadilika kabisa, mapigo ya moyo yanaanza kwenda mbio, jasho linaanza kutililika, kuhisi kuumwa, kubanwa na haja ndogo na mengine mengi. Kuna mtu alisikika akisema “Yaani mimi bora uniue kuliko kunipitisha mbele ya watu eti nikajitambulishe au kuzungumuza chochote wala siwezi”.

Ukweli ni kwamba hakuna mwanadamu asiye kuwa na hofu hasa katika eneo hili sema ni vile tu watu wanavyitofautiana katika kukabiliana na hofu zao mara zinapo wakabili. Pamoja na kwamba kila mtu anakumbana na hofu lakini hofu hii ya kuzungumza mbele ya watu bado ni tishio na kipengele kwa watu wengi duniani. Kitu hiki ndicho kimenifanya nitake kufahamu zaidi kuhusu kisa hiki, hapa ndipo nimekuja na sababu lukuki  zinazowafanya watu wengi wahofie kuzungumza mbele ya watu. Fuatana na mimi sasa;

Hizi ndizo sababu kwanini watu wanahofia kuzungumza kwa mbele ya watu;

1.   DHANA YA KUWA KITOVU CHA USIKIVU (THE IDEA OF BEING THE CENTER OF ATTENTION).

Kitu hiki watu wengi huwafanya wahofie sana pale lilnapokuja suala la kuzungumza mbele ya hadhara. Kwani,  huogopa sana usikivu na umakini kutoka kwa wasikilizaji ambao hutega masikio na kuvuta umakini wa kusikia kutoka kwa mzungumzaji. Kwasababu hiyo mtu anaanza kujiona kama vile hana kitu cha kuzungumza na kuwaambia wasikilizaji wake. Watu wengi hujiuliza na kufikiria sana kuwa watawaambia nini wasikilizaji wao, hasa wakikumbuka macho ya hadhira na umakini wao wa kutaka kujua kutoka kwa mzungumzaji wao.

Kitu kikubwa hapa ni kufanya maandalizi ya kutosha , kujiamini kuwa unaweza na kubwa kuliko ni kuamini kuwa unaweza kufanya hivyo kuliko mtu yeyote hapo, ndiyo maana wanakusikiliza. Ubongo wako ukiuambia hivyo utafanya hivyo kweli si unajua ubongo unafata amri ya mtu mwenyewe.

2.    KIWANGO CHA MAISHA YA WASIKILIZAJI/HADHIRA (STATUS OF AUDINCE).

Watu wale na digrii zao nitawaambia nini mimi, watu wale na pesa zao watanisikiliza kapuku mimi! Maneno kama hayo nikutana nayo kwa baadhi ya watu nilipo wauliza kuhusu jambo hili. Na nimekuja kugundua kwamba kiwango cha maisha ya wasikilizaji (Hadhira) ni moja ya sababu ambayo watu inawapa kiwewe cha kuzungumza mbele ya hadhira. Kutokana na hadhira kuwa na kiwango kikubwa pengine cha elimu, uchumi, akili, maarifa n.k kumzidi yeye, hapa msemaji huzani kuwa wasikilizaji wake wanajua kila kitu na hivyo huhisi kama vile hatoeleweka au pengine kufanya marudio tu na kuwapotezea muda. Hiki kitu siyo kweli kwani hakuna binadamu yeyote ambaye anafahamu kila kitu hayupo na hawezi kuwepo. Mawazo haya nilikuwa nayo pia siku za nyuma nilikuwa nafikiri kuwa, watu wote walioko sekondari wanajua kingereza kumbe ni fikira tu. Hivyo hata wewe ukifikiri kuwa  hadhira wako wanafahamu kila kitu tambua kuwa hizo ni fikira tu.Jiamini wewe na chukulia kuwa ujumbe unaowapelekea hawaujui ndio kwanza unakwenda kuwasomesha.

 3.   HOFU YA KUKOSOLEWA (FEAR OF CRITICISM).

Nimekuja kugundua kuwa asilimia kubwa ya watu wengi hawapendi kabisa kukosolewa, hasa kukosolewa mbele ya hadhira. Wengi wanapenda kusifiwa, kupongezwa, kutambuliwa n.k,  lakini siyo kukosolewa na kuambiwa ukweli. Hivyo watu wa aina hii wakifahamu kabisa kuna watu fulani ni maarufu ka kukosoa na wapo mbele yao, watajitahidi wasizungumze kabisa, kama itawabidi kuzungumza hapo ndipo huwa mwanzo wa hofu na kujawa na wasi wasi mwingi.

 Ndugu katika hili naomba utambue kuwa huwezi kuishinda hofu yeyote kama utakuwa unaikwepa. Fanya kuifata hofu yenyewe,yaani kama ulikuwa unaogopa kukosolewa tafuta sehemu yenye wakosoaji wengi ongea hapo hapo wakukosoe, kama ulikuwa unahofu ya kusungumza mbele ya watu wengi anza kuzungumza mbele ya watu ,kama ulikuwa unahofia kuanzisha biashara anza mara moja  utashangaa hofu itaisha yenyewe tu.

Pia ni  muhimu kutambua kuwa ukosoaji ni muhimu sana katika maisha yetu kwani huu ndiyo huibua makosa ili kurekebisha na kuimalisha katika kila jambo, ndiyo maana kuna msemo unasema criticisim may not be agreeable but its very neccessary it calls attention to unhealthful state of thing. Tafisiri yake ni kwamba “Ukosoaji unaweza usikubalike, lakini ni muhimu sana kwani huleta umakini kwa mambo ambayo hayaendi sawa”. Usipende kuwachukia wanao kukosoa jifunze kutoka kwao. Japokuwa wengine wanaboa kweli kweli. 

4.   HOFU YA KUSHINDWA (FEAR OF FAILURE).

Hiki ni kitu kingine ambacho watu wengine huweka akili na mitazamo yao mikubwa kuwa wakishindwa kufanya vizuri kama watu fulani itakuwaje? Na wengine huwaza kuwa mama yupo, baba yupo, mke, mchumba, mme, rafiki, na watu wengine muhimu kwamba nikishindwa kufanya vizuri kama nilivyo waaminisha itakuwaje? Au wataniona je? Kwa kuwaza hivi watu wengi hujikuta wapo katika hofu ya kupoteza uaminifu, sifa na jina ambalo watu hao wamelijenga.

 Rafiki ukweli ni kwamba hakuna binadamu asiyefanya makosa na huo ndio ubinadamu kama ulikuwa hujui. Nasema kuwa usiogope kukosea kwani hakuna asiye kosea na uzuri ni kwamba “makosa yanatuongezea uzoefu na uzoefu unatupunguzia makosa”.Jinfunze kupitia makosa yako. Waweza bonyeza linki hii

 5.   MAANDALIZI MABOVU (POOR PREPARATION).

Kama ulikuwa hujui ni kwamba “poor preparation prepare poor performance” yaani, “Maandalizi duni huandaa matokeo mabaya”. Huo ni ukweli usio pingika kwamba kadiri unavyofanya maandalizi ya kutosaha na kufanyia mazoezi mengi ndivyo unavyoongeza ujasiri na kupunguza hofu au uoga.

 Katika hili haikikisha kuwa unapohitajika kusimama mbele ya watu pengine kwaajili ya kutoa ujumbe fulani au jambo lolote lile, hakikisha unafanya maandalizi ya kutosha. Hii itakusaidia sana asee.

 6.   MATATIZO BINAFSI (PERSONAL ISSUES).

Saikolojia inaonyesha kuwa malezi na makuzi ya mtu hasa kipindi cha utotoni yana mchango mkubwa sana katika kuathiri akili yake hata anapokuwa mtu mzima. Hii ni sawa na kusema kama umelelewa kwenye familia ya wazazi wakali, wenye kukufokea, walevi,wenye sifa mbaya mtaani, mzazi mmoja,kulelewa na ndugu mfano kaka, shangazi, mjomba,kukukosoa sana, kubaguliwa,kufanyiwa manyanyaso na mateso mengi. Hii husababisha mtu atakapokuwa mtu mzima kujichukia, kutokujiamini, kuwa na aibu sana pia anakuwa mtu wa kujikatia tamaa mapema sana.

 Hapa kuna kitu cha kujifunza, kama mtu ameathiriwa na malezi ya utotoni waweza kubadili mtazamo huo na kujenga mtazamo mwingine tofauti kabisa. Kama tatizo ni kubwa nashauri awaone wataalamu mapema ili aweze kusaidika au waweza kuwasiliana nami kupitia mawasiliano hapo chini.

 7.   KUKOSA KUJIAMINI (LACK OF CONFIDENCE).

Kuna watu automatic tu hawajiamini wao wenyewe. Sasa mtu kama huyu akiwa hajiamini yeye mwenyewe hata linapokuja suala la kuzungumza mbele ya watu  wengine huogopa sana akihofia atawalisha matango poli watu wengine. Ndugu yangu kama hujiamini hili ni tatizo ambalo inatakiwa ulishughilikie mapema sana kabla halijakughalimu.

Kujiamini  ni muhimu sana kwa kila mtu aliyepanga kufika mbali vinginevyo itakughalimu na kukurudisha nyuma katika kuyaendea malengo na ndoto zako na utaishia kuwa mtu wa kawaida tu.

 Ndugu ukweli ni kwamba naweza kuongea mengi sana katika eneo hili. Wacha nimalize kwa kusema kuwa uwasilishaji wa hoja mbele ya watu haupingiki, kwani utafanya biashara utahitajika kuzungumza, utakuwa mwandishi na mwalimu mkubwa bado utahitajika kuzungumza, ukitaka kafanya siasa bado utahitaji kuzungumza, ukitaka kuwa kiongozi kanisani, msikitini, au sehemu yeyote ile bado utahitaji kuwasilisha hoja zako mbele ya watu au mtu mmoja mmoja. Kwa vyovyote vile itakavyokuwa, nipende kukushauri kuwa changamkia na fanyia kazi suala hili kabla maji hayajakufika shingoni. Na mimi sitaki maji yakufike shingoni ndiyo maana nimekuletea chanzo cha tatizo hili si unajua huwezi kutatua tatizo kama hujui chanzo cha tatizo hilo! Vinginevyo itakuwa ni chanzo cha matatizo mengine.

                           Rafiki, ni matumaini yangu kuwa umejifunza kitu.

na kama unachangamoto katika hili pengine namna gani ya kuondokana na adha hii sasa waweza kuwasiliana na mimi moja kwa moja kupitia mawasiliano hapo chini naamini utasaidika.

GeT tO ThE nExT lEvEl!

Makala hii, imeandaliwa na kuandikwa na MIGONGO ELIAS Mshauri & Mwalimu Wa Saikolojia, Uchumi na Maisha. Mwanzilishi na Mwendeshaji wa Mtandao wa addvaluetz. Karibu sana ujiongezee thamani yako. 

Kwa mawasiliano;

Whatsapp & Sim >>+255767653697 /+255783327456

Email>> eliasmigongo120@gmail.com.

Facebook>> MIGONGO ELIAS.

LinkedIn>>Migongoe. 

Pinterest>>eliasmigongo.

Kama umejifunza kitu, niachie maoni yako nitafurahi kujifunza pamoja nawe. 

 

 

 

Popular posts from this blog

GHARAMA 5 ZA KUUFIKIA UKUU UNAOUTAKA.

USIKUBALI KUAJIRIWA KABLA HUJASOMA HAPA.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.