HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 23.

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 23. Ilipoishia...... Alipofika nje, alimkuta Elimina katahamaki sana tena anahasira sana.  "Umefanya nini Elvine? Elimina aliuliza kwa ukali sana tena hadi macho yalikuwa mekundu kama damu kwaajili ya kujaa hasira.... Swali; kwanini Elimina anahasira? Na Elimina huyu anasiri gani na nyumba iliyoungua moto? Kusoma sehemu ya 22 bonyeza hapa   Sasa inaendelea...... Elvine alikuwa anatetemeka  kwa hofu ya yale anayoyaona lakini alistaajabu kuona ni kama mkewe hajali sana kuhusu yeye. Alimtazama kwa makini sana mkewe akiwa anajaribu kutafakari kwanini anaonekana kuwa na hasira juu yake. Elimina akajishitukia "Hey, wewe! Nini sasa unanitazama hivyo?" "Nakutafakari sipati majibu!' "Nimefanyaje kwani?" "Hamna ila sijajua kama umenihofia mimi au hilo swali lako linamaana gani? "Elvine baba sina maana hiyo uliyoelewa wewe kabisa. Shida yangu mimi umefanya nini mpaka unataka kuhatarisha maisha Yako namna hii. Hujui namna ga

GHARAMA 5 ZA KUUFIKIA UKUU UNAOUTAKA.

GHARAMA 5 ZA KUUFIKIA UKUU UNAOTAKA.

 “Ukiona vya elea, ujue vimeundwa.” “Hakuna vya bure duniani.” “Mkono mtupu haulambwi.”  Hizi ni baadhi ya kauli ambazo zimeenea karibia kila kona ya dunia. Na lengo lake si kutukomoa au kutusema vibaya, laah hasha! Bali  ni kutaka kutuonyesha kuwa katika kuyafikia mafanikio tunayoyataka ni lazima tulipe gharama. Kumekuwa na kasumba ya watu wengi sana kutamanani mafanikio makubwa na kufika mbali sana katika maisha yao. Lakini pamoja na kutamani huko, asilimia kubwa ya watu bado kuufikia ukuu wanao utaka imekuwa ni gumuzo mtaani.

Watu wengi wanatamani sana mafanikio ya baadhi ya watu maarufu na waliofanikiwa katika maisha yao au kutimiza ndoto zao. Na hapa wengi wamekuwa wadau na wapambe wa mafanikio ya watu waliofanya vizuri kwa nafasi zao. Wakati huo, huwa wanaona kama watu wengine wanabahati, wamezaliwa na na neema kuliko watu wengine, na mara nyingi wameyachukulia maisha kuwa ni simpo sana. watu wa namna hii, huchukulia mafanikio ni kitendo cha siku moja.  Hayo yote sikatai lakini, ni muhimu tufahamu kuwa mambo huwa hayatokei yenyewe tu kama wengi tunavyodhani. Ni lazima uyafanye yatokee yaani, you must make them happen.

Kunaupande mmoja wa shilingi ambao watu wengi linapokuja suala la mafanikio huwa wanasahau kabisa kuuzungumzia. Na upande huo ni ulipaji wa gharama juu ya ndoto na malengo yetu katika kuyafikia. Na gharama utakayo kuwa tayari kuilipa ndiyo itaonyesha ni matokeo kiasi gani unakwenda kuyapata. Wengi tunamfahamu Yesu kuwa alikuwa ni mtenda miujiza lakini nyuma ya kutenda miujiza hiyo ni wachache waliofahamu siri na gharama zake. Ambapo wakati mwengine ilimlazimu kufunga, kukesha, kuomba, na mengine kibao ili kufanya miujiza hiyo, kitu ambacho wengi wanataka tu kuona matokeo lakini hawataki kabisa kuufuata mchakato wa kuufikia ukuu wenyewe.

Hapa nimekuuandalia gharama tano unazopaswa kuzilipa katika kuufikia ukuu unao utaka katika maisha yako. Gharama hizi pia, zimezungumzwa na waandishi mbali mbali akiwemo Godius Rweyongeza katika kitabu cha jinsi ya kufikia ndoto zako. Na wewe, ni muhimu kuzifahamu ili uanze kuzichukua mapema. Gharama hizi ni pamoja na;

 Ya kwanza ni:

Gharama ya kujifunza. Ni kweli watu wanatamani sana kufanikiwa katika maeneo mbali mbali pendwa ya maisha yao. Lakini ajabu ni kuwa, watu hawa hawako tayari kabisa kulipa gharama  ya kujifunza. Kunamsemo mmoja naupenda nao unasema “Continous learning is the minimum requrement of success in any  field ”

Yaani, “kujifunza kwa mwendelezo ni hitaji la chini la mafanikio katika eneo lolote”. Hiii ni sawa na kusema, kama unataka uwe mfanyabiashara bora jifunze zaidi kuhusu biashara, kama unataka uwe mtaalamu wa afya jifunze zaidi kuhusu afya, vivyo hivyo kwa wachezaji, waimbaji, mainjinia, n.k. na hapo waweza kuweka mkakati wa kujifunza kitu kipya kila siku katika eneo husika utashangaa utakavyo kuwa mbobevu katika eneo hilo.

Ya pili ni:

Gharama ya kuacha baadhi ya vitu. Hapa ni pagumu kidogo, kunanamna mtu anakuwa anatamani kuwa mtu fulani hivi lakini, jinsi anaishi sasa ni tofauti kabisa. Kitu hiki kimefanya watu kuwa na tabia nyingi sana ambazo zinawasaliti kuuelekea ukuu wao. Kunausemi maarufu katika eneo hili nao unasema “inorder  to get into something new you will have to get out from something old else well” yaani, “ilikuingia kwenye kitu kipya ni lazima utoke kwenye kitu cha zamani pia”. Kunatabia, marafiki, au wakati mwengine ni vitu pendwa kwako vitakubidi uvitoe ili kuufikia ukuu unaotaka. Mfano ukitaka uishi chini ya pato lako kunatabia, marafiki au vitu itakubidi uachana navyo kwanza mf. Tabia ya ulevi, ununuzi vitu holela n.k. yaani kiufupi kufanya maajabu ni kufanya vitu tofauti na wengine.

Ya tatu ni:

Gharama ya fedha. Nikili tu kusema kuwa, gharama hii watu wengi wanaifahanu sana. Sema ni vile tu watu wanaamini kuwa kunasiku moja mambo yatajipa yenyewe tu. Ukweli ni kwamba, kunawakati ndoto yako itakuhitaji ulipie gharama ya fedha kama kulipia mafunzo, waalimu, mtaji na vitu vingine husika. Watu wengi hawako tayari kuilipa gharama hii, huku wakitegemea kuamka mambo yametiki yenyewe. Hapa ni kuambia tu ndugu yangu utasubiri sana na pengine huenda ukaenda kuyanufaisha makaburi

Ya nne ni:

Gharama ya muda. Gharama hii pia inajulikana na watu wengi, sema watu wengi ukiongea nao huonekana kuwa bize sana hata kwa mambo ambayo hayako bize. Uzuri ni kwamba, watu wote hupewa saa 24 kwa siku, shida inakuja kwenye namna ya kuzitumia saa24 hizo na kuweka vipaumbele. Wengi hulalama na kudai kuwa hawana muda wa kutosha. Huku ni kukwepa majukumu yao waziwazi. Ifahamu ndoto yako, tambua na fahamu ni muda kiasi gani unautenga kwaajili ya ndoto yako kisha, fanyia kazi kila siku. Usianze kulalamika kama wengine wafanyavyo.

Ya tano ni:

Gharama ya kuchukua hatua ya kufanyia kazi. Pamoja na kuwa baadhi ya wengi kufahamu wao ni akina nani katika safari ya mafanikio yao. Kufahamu wanakoelekea, mikakati na njia za kuelekea huko. Lakini bado wengi suala la kuchukua hatu ya kufanyia kazi bado ni tatizo. Tunajua umefundishwa kwenye semina, kanisani, nyumbani, na sehemu zingine kwamba yapi yakupasayo kutenda lakini kuchukua hatua na kutenda bado ni kimbembe  kwa waswahili wengi. Hata hivyo, kama unataka kuufikia ukuu unao utaka hakuna namna ukafanya kazi tena kwa bidiii, yakupasayo kutenda. Si unajua matendo yanasauti kuliko hata maneno yenyewe.

 Ndugu yangu zipo gharama yingi sana kuelekea ukuu unao utaka kutegemeana na hitaji lako na aina ya gharama itakayokuhitaji kuichukua. Na tambua wazi kuwa, malengo na ndoto kubwa zinahitaji gharama kubwa pia. Na kadiri utakavyo zifahamu gharama zinazotakiwa kuzilipa yakupasa ufanye hivyo mapema sana. kwani, wepesi wa kutambua gharama za kulipia na kuanza kuzilipa ndivyo utakavyofanya haraka kuufikia ukuu wako. Fanya hivyo mapema fanyia kazi, acha maneno  badala yake fanya kwa vitendo  hakika tutakutana kwenye meza moja ya wanamafanikio tukiufurahia ukuu weneyewe.

Rafiki, ni matumaini yangu kuwa umejifunza kitu.

na kama unachangamoto katika hili pengine namna gani ya kuondokana na adha hii sasa waweza kuwasiliana na mimi moja kwa moja kupitia mawasiliano hapo chini naamini utasaidika.

GeT tO ThE nExT lEvEl!

Makala hii, imeandaliwa na kuandikwa na MIGONGO ELIAS Mshauri & Mwalimu Wa Saikolojia, Uchumi na Maisha. Mwanzilishi na Mwendeshaji wa Mtandao wa addvaluetz. Karibu sana ujiongezee thamani yako. 

Kwa mawasiliano;

Whatsapp & Sim >>+255767653697 /+255783327456

Email>> eliasmigongo120@gmail.com.

Facebook>> MIGONGO ELIAS.

LinkedIn>>Migongoe. 

Pinterest>>eliasmigongo.

Kama umejifunza kitu, niachie maoni yako nitafurahi kujifunza pamoja nawe


Popular posts from this blog

USIKUBALI KUAJIRIWA KABLA HUJASOMA HAPA.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.