HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 31
Moja ya ujuzi muhimu sana ambao kila mtu ningependa awe nao katika nyakati hizi ni commmunication skill. Huu ni uwezo wa kuwasilisha ujumbe na mawazo yako mbele ya watu, na watu wakakuelewa. Na, hii inaweza kufanyika kwa kutumia maandishi (writing skill), kuzungumza (speaking skill), kusikiliza kwa makini (listening skill) n.k.
Juzi kama hizi ni muhimu sana kwa kila mtu. Kwani,
zitaongeza thamani na uhusiano wako na watu wengine. Leo tunaenda kuutazama
ujuzi mmoja utakao ongeza thamani na mahusiano yako na watu wanao kuzunguka. Na
ujuzi huu ni ujuzi wa kusikiliza kwa makini yaani, active listening
skill. Ukweli ni kwamba, kumekuwepo na wimbi kubwa sana la watu kutaka kuongea tu na kusilizwa muda wote. Pasipo wao kuwasiliza watu wengine .
Kuna namna saikolojia inaeleza kuwa mtu anaposikilizwa kwa makini hasa anapojielezea na kueleza mambo yake ya moyoni, huwa anajisikia vizuri sana kupata burudiko la moyo. Hali hii, humfanya ajione mwenye kuthaminiwa na kupendwa kweli kwel.
Katika
hili, changamoto bado ni kubwa sana. Kwani, watu wengi bado hawajajua
kusikiliza ingawaje wapo vizuri kwenye kuongea. Kitu hiki ni kidogo sana. Lakini,
usipojifunza kusikiliza kwa makini na
kuepuka kuwaingilia wengine katika mazungumzo utashusha brand yako rafiki. Na, hapa nikafikiria
na kuona kuwa watu wengi wanafanya hivyo pengine, ilikuwafurahisha wasikilizaji, ilikuonekana kuwa wanajua vitu vingi sana pamoja na hayo pengingine hawajajua umuhimu na faida ya
kusikiliza kwa makini. Nipo hapa, naenda kukupa faida kabambe za kuwa
msikilizaji mzuri, ambazo ni;
Faida ya kwanza:
Utaokoa muda na kuelewa haraka.
Usipokuwa
msikilizaji mzuri uwe na uhakika wa kupoteza muda mwingi sana katika mazungumzo
yako na watu wengine na kushindwa kuelewa haraka kile kilicho kusudiwa. Kitu hiki hutokea sana pale munapokuwa watu wengi kidogo mada ikiwekwa mezani utashangaa
kuona kila mtu akizungumza bila utaratibu wowote yaani, inakuwa kelele badala
ya maongezi. Na, mbaya zaidi si kwamba anaongea vitu vya kueleweka no, ni vile
tu anataka kuonekana kuwa anazungumza. Kitu hiki utajikuta mmepoteza muda
mwingi sana. Je unataka kusikilizwa? Basi wasikilize wengine kwanza. Hapa si
kwamba tu mtaokoa muda bali mtaelewana mapema pia.
Faida ya pili.
Utajenga heshima na uaminifu.
Tambua
kwamba, watu wana vitu vingi sana ndani ya mioyo yao. Sema hawana watu wa kuwaeleza
watu wenyewe ndo hao wanataka kuongea muda wote. Kama ni kiongozi atataka
aongee muda wote, kama ni baba atataka aongee muda wote, kama ni mfanya biashara
atataka aongee muda wote, kama ni mke atataka aongee muda wote tena ana taka
asikiliwe kwa makini hali na huku hataki kabisa kuwasikiliza wengine. Kitu hiki
kitapunguza imani na heshima kwa anaye eleza haja zake. Watu hujisikia amani na
kuhisi wapo sehemu salama pale wanapo pata watu wa kuwasikiliza. Hivyo chagua
kuwa msikilizaji mzuri watu watakuheshimu na kukuamini pia.
Faida ya tatu.
Utapata nafasi ya kujifunza zaidi.
Kuna
msemo mmoja naupenda sana ambao unasema “when you talk you’re only repeating what you’re
already know. But, when you listen you’re giving yourself a chance to learn
something new” yaani, ukiwa unaongea unakuwa unarudia tu kile ambacho tayari
unakifahamu. Lakini, ukisikiliza unajipa nafasi ya kujifunza kitu kipya.
Hivi ulishawahi kukutana na mtu unamweleza inshu yako lakini, huku anaitikia na kusema tupo sawasawa, hali huku unamuona kabisa anachati na kucheka cheka na status tu? Ukimaliza kuzungumza anakuuliza umesemaje kweli? Binafsi nimeona wengi sana, ndipo nilipogundua kuwa kunashida mahali. Utakuta mtu amekuita na kukusubirisha huku akipigiwa simu anapokea na kuanza kuongea na kucheka bila hata kutaka radhi.
By the way utakuwa umebeba mambo mengi kwa wakati mmoja niseme tu kwamba kujifunza na kuelewa kwako kutakuwa ni kugumu sana. Na, matokeo yake utakuwa umetoka hola. Usiwe kama watu wengine wape watu masikio yako wanavitu vingi vya kukufundisha lakini kuwa makini kuchambua yakufaayo. Wakati wa kusikiliza sikiliza wakati wa kuchati chati kweli kweli na utajifunza mengi.
Faida ya nne:
Utaondoa mitazamo hasi juu ya wengine.
Kuna watu ni wazuri sana wa kuhukumu watu wengine. Hapo akiona au kuhisi kitu fulani
tu kuhusu mtu fulani utasikia anahukumu hata kwa vitu ambavyo siyo kweli. Kuna watu
kwa kuwatazama tu watu fulani fulani hivi, wamewaita wezi, wamewaita makahaba,
wamewaita wachoyo, wamewaita masikini, wamevumisha kila uvumi, mtaani. Ndugu, kutokana na uwezo wa kusikiliza kwa makini utakuja kushangaa
kama ukikaa chini na kuwasikiliza watu utakuta wana mambo makubwa sana nyuma ya
pazia. Hivyo jitahidi kuwasikiliza watu kwa makini na achana na habari za kuwahukuma na ukuwapa mitazamo hasi wengine wewe siyo Mungu.
Faida ya tano.
Kuboresha mahusiano yako na watu wengine.
Kama utakuwa msikilizaji mzuri utajikuta, watu wanakuamini, wanakuheshimu, wana
kuthamini, utawaelewa haraka na hii italeta ushirikiano hasa katika kubeba
changamoto zilizojitokeza kwa mzungumzaji. Kitu hiki peke yake tu kitaongeza
sana uhusiano wako na watu wengine hivyo
jitahidi kuwa msikilizaji mzuri watu watakuamini, kukuheshimu na kukuthamini na
hapo ndipo mahusiano yako na wengine yatakaa poa.
Mwisho kabisa tuelewe kuwa, kusiliza
kwa makini ni ujuzi ambao angalau kila mtu na shauri ajifunze. Na hapa utafahamu
sababu ya mtu kuwa na masikio mawili na mudomo mmoja ni kwamba anatakiwa
kusikiliza mara mbili ya anavyoongea. Ingekuwa ni kwa kimombo ningesema the
reason why we’ve two ears na one mouth is that we can listen twice as much as
we can speak. Hapa ninasema wasikilize watu, acha kuchati wakati wa mazungumzo,
usiingilie mazungumzo ya mtu subiri amalize kwanza kama unacha kuongezea au kuuliza,
kupinga. Na wewe usikubali mtu akuingilie unapo zungumza. Lakini, sharti ni
kwamba, lazima na wewe usiwaingilie kwanza wengine. Unataka watu wakusikilize? Wasikilize
wewe kwanza. Unataka watu wasikuingilie kwenye mazungumzo usiwaingilie wewe
kwanza. sikiliza kwa makini. Si unajua what goes arround comes around eeh?
Rafiki, ni matumaini yangu kuwa umejifunza
kitu.
na kama unachangamoto katika hili pengine
namna gani ya kuondokana na adha hii sasa waweza kuwasiliana na mimi moja kwa
moja kupitia mawasiliano hapo chini naamini utasaidika.
GeT tO ThE nExT lEvEl!
Makala hii, imeandaliwa na kuandikwa na MIGONGO
ELIAS Mshauri & Mwalimu Wa Saikolojia, Uchumi na Maisha.
Mwanzilishi na Mwendeshaji wa Mtandao wa addvaluetz. Karibu
sana ujiongezee thamani yako.
Kwa mawasiliano;
Whatsapp & Sim >>+255767653697
/+255783327456
Email>> eliasmigongo120@gmail.com.
Facebook>> MIGONGO ELIAS.
Facebook page>>Add Value Network.
LinkedIn>>Migongoe.
Pinterest>>eliasmigongo.
Kama umejifunza kitu, niachie maoni yako
nitafurahi kujifunza pamoja nawe.