HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 31

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 31 Ilipoishia………. Elvine alipoteza amani kuliko hata mkewe maana kila alipomtazama mkewe basi moyo wake ni kama ulikuwa unachomwa na mwiba uliojishikiza huko kwenye mishipa ya moyo. Nafsi yake ilitaabika na ndipo alipoamua kutafuta muda mzuri, baada ya chakula cha jioni, azungumze na mkewe, maana ule ukimya wa siku mbili ulikuwa adhabu kubwa sana kwake. Kusoma sehemu ya 30 bonyeza hapa Sasa inaendelea………. Elimina mamy naomba kujua kwanini hutaki kuniuliza kuhusu sababu ya haya yote? Maana najua unajua kuwa kuna mahali mimi nilikosea, sasa unapokaa kimya hivyo… kiukweli unazidi kunichanganya maana ni kama hutaki kujua, sasa unadhani mimi roho yangu itatulia kweli?. Hata kama ungekuwa wewe lazima usingepata amani, ungekuwa hata unawaza hivi nakuwaziaje, nakuonaje na ninajisikiaje ninapokuona, sasa kwanini wewe umekaa kimya, sema neno tafadhali? (Elvine alikuwa akiongea bila kumtazama mkewe usoni maana moyo wake haukuwa katika hali ya utulivu). Pamoja na ...

NJIA TATU ZA KUKUSAIDIA KUISHI KWENYE DUNIA YA WATU WA BAYA.

 

           

NJIA TATU ZA KUKUSAIDIA KUISHI KWENYE DUNIA YA WATU WA BAYA.

Siku moja nilikutana na mtu mmoja, nikawa naongea nae mawili matatu kuhusu maisha kwa ujumla. Katika mazungumzo yetu ambayo yalikuwa moto sana. Kwani, mada hiyo ilikuwa nzuri  haswa.

Lakini katika mazungumzo yale, niligundua kuwa, jamaa alikuwa anayalalamikia sana maisha. Akidai kuwa vyuma vimekaza, maisha magumu, maovu yamezidi, watu, siyo waaminifu, watu ni wabaya sana na malalamiko mengine kibao. Siwezi kuandia yote hapa lakini mazungumzo yaliendelea na yalikuwa mazuri sana.

Kuna baadhi ya mambo sikukubaliana kabisa na huyo mtu. Lakini, mengine niliunga hoja mkono. Na moja wapo ni kwamba tunaishi kwenye dunia ambayo ipo kasi  sana, imejaa maovu mengi, ina wetu wema na wabaya n.k. katika huuhuu ulimwengu wa maasi na maovu mengi, ndimo humo humo watu wema wanapatikana, humo humo na wewe unaishi, hata mimi halikadharika naishi humu duniani ambamo hata wewe unaishi.

Mara nyingi  tumeambiwa tujitenge na watu wabaya, watu hasi yaani ambao hawanafaida kwetu. Ni kweli sikatai, lakini jambo hili ni gumu kidogo. Sababu tunaishi kwa dunia ambayo kila siku tunakutana na watu ambao tunaweza kuwafahamu ama laah! Na hao wanawezakuwa wema au wabaya, waaminifu au wasaliti, waongo au wakweli. Ni ngumu kuwatambua moja kwa moja kwani, wengi wao huvaa ngozi za kondoo kumbe ni mbwa mwitu. Kiufupi tunaishi kwenye dunia ambayo, watu wengi tulioambiwa ni wema, kwakweli wengi wao si wema ni wabaya kabisa. Watu wengi tulioambiwa ni wabaya kwakweli wengi wao si wabaya ni wema sana.

Kwa vyovyote vile hawa watu tunaishi nao hapahapa duniani, na wakati mwingine watu hao hao Mungu huwatumia kutubarikia, na  shetani harikadhalika huwatumia kuwatesa watu wengine. Sasa tukisema tujitenge na watu hawa itakuwa ngumu, vinginevyo itabidi kutengeneza katika kadunia kengine tofauti na hii dunia. Ndiyo maana biblia inasema,  mimi siombi kwamba uwatoe katika ulimwengu; bali uwalinde na yule mwovu” (yohana17:15). Sasa kama hatuwezi kuwakwepa hawa watu ni muhimu sana tukajifunza namna gani tukaishi nao katika dunia hii. Soma njia hizi tatu zitakusaidia sana.

NJIA YA KWANZA: JAA MAARIFA SAHIHI.

Karne hii tunaishi kwenye ulimwengu wa taarifa yaani, information age. Ambao ni tofauti kabisa na zama zilizo pita, zama kama za kutumia nguvu, ambapo watu wenye nguvu ndiyo walichukua nafasi na kuwa watu wakubwa. Lakini sasa, watu walio na wengi wa maarifa na taarifa katika eneo fulani ndio huwa watawala na wakuu katika eneo hilo. Hivyo hata wewe ukitaka ushinde katika ulimwengu huu yakupasa uwe mtu wa taarifa na maarifa . maarifa safi na sahihi hapo ndipo utakapo jua kutofautisha x na +. Kiufupi ndugu unahiitaji maarifa sahihi kuhusu roho yako, maarifa sahihi kuhusu afya yako, maarifa sahihi kuhusu akili yako, maarifa sahihi kuhusu kuhusu uchumi wako, maarifa sahihi kuhusu maendeleo yako n.k vinginevyo utakwenda na maji.

NJIA YA PILI: KUWA WEWE.

Kwasababu ya mfumko wa wingi wa maarifa katika karne hii, watu wengi wamekuwa wakiishi maisha ya kuiga kutoka kwa watu wengine, pengine kwa kuwaona mtandaoni au  kukutana nao pengine kutokana na umaarufu wao, watu wengi huacha uhalisia wao na kuishi maisha ya waengine. Hapo ndipo utakuta ameona watu wanaiba na yeye anaanza kuiba, anaona watu wana danganya anaanza kudanganya, ameona watu wanaishi maisha fulani anataka na yeye aishi maisha yale. Ukiwa mtu wa namna hii ndugu kwa dunia hii, ni kuambie tu kwamba utakwenda na maji.

NJIA YA TATU: WASIFIE KWA MAZURI YAO.

Pamoja na kwamba tunaishi na watu wabaya (Negative people), utakuja gundua watu hawa si wabaya kwa 100%, kwa namna moja au nyingine kuna mazuri mengi sana wanayo. Tena, tukiyafahamu yanaweza kuwa ni msaada na faida kwa maisha yetu. Si unajua dunia ni duara! Utakuja shangaa uliye mkataa na kumkimbia ndo huyo huyo ukakutana naye kwenye shida zako. Halafu kitu hii, inashangaza usiombe kukutana nayo. Hapa nacho taka kukazia ni kwamba, usiwe mwepesi wa hukumu watu kwa makosa yao ya zamani au ya sasa,  usikariri watu hubadilika, na kuwa tufauti kabisa na vile unawafahamu.

Badala ya kujitenga na kuwakimbia watu wabaya wakati mwingine jifunze kuuona uzuri wao na kuufunua kwao na pengine wanafanya mabaya hayo kwa kuwa hawajui kuwa wao ni watu muhimu sana kwenye familia, jamii, nchi na dunia kwa ujumla. Wasifie kwa mazuri yao pengine watajitambua na kubadilika kabisa, binafsi njia hii nimeitumia sana na wengi wamebadilishwa na njia hii, kwa kujua nafasi yao, nini wamebeba na wanaweza kuleta matokeo gani kama watautumia uwezo wao.

Ndugu, kwa namna yeyote ile yaani, utake usitake utakutana na watu wazuri kwa wabaya, waongo kwa wakweli, waaminifu kwa wasaliti. Hivyo usipo kuwa na maarifa sahihi, kujitambua na kuwa wewe wakati mwingine kutambua umuhimu wa watu unao kutana nao itakuwa ni changamoto sana kuishi katika dunia hii. Lakini, kama utatumia njia walau hata moja tu hapo juu utakuwa ni mtu wa tofauti sana.

 Lakini ifahamike kuwa kwakuwa tumeona kuwa kujitenga na watu wabaya ni ngumu. Hii isiwe ni tiketi ya kung’ang’a nia watu ambao hawana tija katika maisha yako, hivyo ni muhimu kutambua wewe ni nani umebeba nini, watu gani wa kuambatana nao na wapi siyo.  Katika hili watu wabaya kujitenga nao ni ngumu lakini sikushauri uambatane nao. Si unajua kuna kujitenga na kuambatana eeh.

Rafiki, ni matumaini yangu kuwa umejifunza kitu.

na kama unachangamoto katika hili pengine namna gani ya kuondokana na adha hii sasa waweza kuwasiliana na mimi moja kwa moja kupitia mawasiliano hapo chini naamini utasaidika.

GeT tO ThE nExT lEvEl!

Makala hii, imeandaliwa na kuandikwa na MIGONGO ELIAS Mshauri & Mwalimu Wa Saikolojia, Uchumi na Maisha. Mwanzilishi na Mwendeshaji wa Mtandao wa addvaluetz. Karibu sana ujiongezee thamani yako. 

Kwa mawasiliano;

Whatsapp & Sim >>+255767653697 /+255783327456

Email>> eliasmigongo120@gmail.com.

Facebook>> MIGONGO ELIAS.

LinkedIn>>Migongoe. 

Pinterest>>eliasmigongo.

Kama umejifunza kitu, niachie maoni yako nitafurahi kujifunza pamoja nawe. 

 

Popular posts from this blog

MAAJABU YA AKIBA

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 29

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 27.