HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 31

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 31 Ilipoishia………. Elvine alipoteza amani kuliko hata mkewe maana kila alipomtazama mkewe basi moyo wake ni kama ulikuwa unachomwa na mwiba uliojishikiza huko kwenye mishipa ya moyo. Nafsi yake ilitaabika na ndipo alipoamua kutafuta muda mzuri, baada ya chakula cha jioni, azungumze na mkewe, maana ule ukimya wa siku mbili ulikuwa adhabu kubwa sana kwake. Kusoma sehemu ya 30 bonyeza hapa Sasa inaendelea………. Elimina mamy naomba kujua kwanini hutaki kuniuliza kuhusu sababu ya haya yote? Maana najua unajua kuwa kuna mahali mimi nilikosea, sasa unapokaa kimya hivyo… kiukweli unazidi kunichanganya maana ni kama hutaki kujua, sasa unadhani mimi roho yangu itatulia kweli?. Hata kama ungekuwa wewe lazima usingepata amani, ungekuwa hata unawaza hivi nakuwaziaje, nakuonaje na ninajisikiaje ninapokuona, sasa kwanini wewe umekaa kimya, sema neno tafadhali? (Elvine alikuwa akiongea bila kumtazama mkewe usoni maana moyo wake haukuwa katika hali ya utulivu). Pamoja na ...

UMEPOTELEA WAPI?

 

UMEPOTELEA WAPI?

Goja nikufikirishe na kukutakafakarisha  kwanza nadhani utanielewa vizuri kile nataka nikueleweshe. Hivi, ulishawahi kuona mtu ambaye alikuwa amefanikiwa sana pengine alikuwa tajiri sana katika maeneo yenu? Lakini, saivi ni mtu wa kawaida sana, ulishawahi kuona mtu aliyekuwa mchezaji mkubwa na maarufu sana siku za nyuma, lakini siku hizi ni mtu wa kawaida sana? Vipi kuhusu wakulima wakubwa, wakubwa? Okey, utasema mara ooh! Mimi ni mtu wa mjini shambani tatizo, au basi! Vipi kuhusu wafanya biashara wakubwa? Viongozi wakubwa na wenye ushawishi mkubwa?  Vipi wakufunzi na waalimu bomba? Kutaja yote ni ngumu sana. 

Lakini, ukiangalia kwa namna ulivyokuwa unawafahamu watu hawa, walikuwa ni watu wenye mafanikio walau makuwa kila mtu katika eneo lake. Kitu cha kushangaza ni kwamba, maisha ya watu hawa kwa sasa ni ya kawaida sana. Pengine wengine walisha geuka na kuwa machokoraa mtaani, wengine wakabaji, wengine matapeli, wengine omba omba. Yaani, maisha yao yamechuja kweli kweli. Si kwamba tuna wadadsi lakini, tunataka tuone watu wa namna hii, pengine kunakitu cha kujifunza kutoka kwao. Swali la kujiuliza watu hawa Walikwama wapi? na wamepotelea wapi?

Lakini, ukiangalia upande mwingine wa shilingi kuna watu ambao mimi kama mimi toka nimewafahamu na kwa mafanikio yao wako nayo vilevile na huku wanazidi kuchanja mbuga kwenda hatua ya mbali sana kwenye maendeleo na mafanikio yao binafsi. Watu  wa namna hii, kuna namna wako vizuri, wanaupiga mwingi na wanastahili pongezi zao. Kwani, uhalisia jambo hili siyo jepesi kama unavyo dhani. Ingawaje ni rahisi sana kama utazifahamu na kuzijua siri za kufanya hivyo. Na hapa ninao uhakika kuwa utakapomaliza tu kusoma hapa utafahamu vitu vingi sana na hautabaki kama ulivyo.

Twendelee  kutafakari kwanza. Vipi ulisha wahi kuona au kusikia watu wa aina hii? Wanakuwa na mipango mingi mingi sana na wanakua wepesi sana wa kuifanyia kazi, na wanaanzisha vitu vingi vingi sana kwa pamoja. Utasikia amefungua mgahawa baada ya mwezi ashafunga, anafungua kibiashara ya duka baada ya wiki mbili ana funga, anaanza kusoma baada ya muda kidogo ashaacha shule, anaanza kulima baada ya muda kidogo asha piga chini, anapata kazi fulani lakini baada ya muda kidogo ashaacha, anaanza uandishi baada ya muda anapotea kwenye ramani, anaanza kufundisha na kufanya uneni baada ya muda anatuacha solemba, kutaja yote muda hautoshi ndugu yangu. Lakini, sasa nadhani umeanza kupata picha eeh! Lakikini swali la kujiula watu hawa wanapotelea wapi?

Kitu hiki ndicho kimenisukuma kuandika leo hapa ambapo ni uhakika kuwa kunakitu utapata. Kiujumla hakuna mtu asiye penda kufanikiwa. Na watu karibia wote wanatamani sana kufanikiwa, na kuwa watu wakubwa, maarufu, wenye heshima na mengine kama hayo. Ajabu ni kuwa hawa watu hawawi kabisa kama wanavyotaka wao. Hii ni pamoja na kwamba, watu wengi  wapo tayari kufanikiwa na kuwa watu maarufu, wenye ushawishi, wenye kugusa maisha ya watu n.k. lakini, watu hao hao hawako tayari kabisa kuufuata mchakato wa kuwa watu ambao wanataka wawe. Yaani, mtu anatamani tu aamke asubuhi tayari ameshakuwa mtu heavy ndani ya usiku mmoja. Hivi kitu hiki kinawezakana kweli jamani? Kama ni sawa itakuwa tumerahisishiwa sana lakini kama siyo kweli ni muhimu kufikiri tena yaani nasema, think again.

Kuna kanuni moja ambayo watu wengi huivunja pindi wanapo taka kufanikiwa na kuwa watu maarufu  badala yake wanakuwa watu wa kawaida sana. kanuni hii ukiifahamu kwa kweli ukichanganya na kanuni zingine za mafanikio ambazo umewahi kufundishwa kutoboa ni swala la muda tu.  Na kanuni hii, itakupa kujulikana na kukutambulisha kwa haraka sana tofauti na unavyofikiria. Nayo si nyingine bali inaitwa,

Kanuni ya mwendelezo(consistency). Wakati mwingine inaitwa copound effect. Kanuni hii inamtaka mtu kufanya kitu kilekile kwa mwendelezo yaani, mara kwa mara bila kuacha. Kitu hiki watu wengi wanakivunja na kupelekea kuanzisha vitu kwa muda tu kisha kuachana navyo. Hali hii, hupelekea wawe watu wa kuanzisha vitu vipya kila siku , huku wakiendelea kujitafuta kila siku, na hawajajipata bado.  Pamoja na kuwepo kwa sababu nyingine nyingi za kusababisha watu kutofikia malengo yao na kuanzisha vitu vingine vipya bila kufanikiwa. Kukosa mwendelezo  imekuwa ni moja ya sababu zinazo wakwamisha watu wengi sana. wakati mwingine kanuni hii, inawataka watu kufanya vitu kwa muda mrefu  bila kuacha kabla ya kuanza  kuonekana.

Goja nikuambie kitu kimoja muhimu hapa nacho ni kwamba, kuanzisha kitu chochote kile, hilo ni jambo la kwanza lakini kukisimamia na kukiendeleza kitu hicho ni jambo lingine tofauti kabisa. Tena wakati mwingine kuanzisha kitu ni jambo jepesi sana lakini, kukiendeleza kitu hicho inahitaji nidhamu ya hali ya juu sana. Vinginevyo itabaki story tu. Utarudi kuwa mtu wa kawaida sana. Sijui kama unaelewa!?

Tafiti zinaonye kwamba, kila kunapo anzishwa vitu au biashara 100 ndani ya mwaka mmoja biashara ambazo huendelea na kufanikiwa huwa ni asilimia 5% tu. Huku 95% hufa na kupotea kabisa. Mfano watu 100 wakaanzisha makampuni ya sabuni  ndani ya mwaka mmoja zitabaki kampuni 5 tu. Na kampuni 95  hubadilishwa, hufa na kubaki maghofu tu. Swali kubwa la kujiuliza kwanini watu wengi hukosa mwendelezo na kufanya vitu kwa muda tu? Au wanakwama wapi? Sasa hapa naenda kukupa sababu kadhaa kwahiyo twende pamoja..

SABABU ZINAZO WAFANYA WATU WENGI WAKOSE MWENDELEZO NI;

1.   Tabia ya kutaka kufanikiwa ndani ya usiku mmoja. Kitu hiki watu wengi kimewandanganya baada ya kudhani kuwa mafanikio ni kitendo cha kufumba na kufumbua tu. Hasa wakiwaona watu wengine walivyo na biashara kubwa, magari mengi, ushawishi mkubwa wanajua kuwa hiki kitu walikipata kwa muda mfupi tu. Haili hii, huwapelekea wanakata tamaa na wanashindwa kuendelea mbele. Wewe usiwe mmoja wao.

2.   Wanataka kuonekana na watu (attention seekers). Hawa ni watu ambao wao huishi kwa kutegemea sana mawazo ya wengine na utakuta mtu, anafanya vitu kwa kuangalia watu wengine wanasemaje. Lengo lake ni kutaka kusifiwa na kuheshimiwa sana.  Hivyo, watu kama hawa kuna vitu kama, kampuni, biashara, na mambo mengine walianzisha ili kusifiwa na watu fulani fulani hivi lakini, kwa bahati mbaya sana watu walipoacha kuwasifia waliacha mara moja na kutafuta kitu kingine watakacho sifiwa nacho. Tabia hii, haitakufikisha popote kwanza inaashiria tu kwamba mtu huyu hajitambui bado.

3.   Kushindwa mara kwa mara huko nyuma. Hisitoria ya kushindwa yaani, kufeli mara kwa mara huko nyuma watu wengi huwafanya waweze kuwa na mtazamo hasi, woga kupita kiasi na kukosa ujasiri wakufanya kitu husika kwa mwendelezo wakijua kuwa napo watafeli tu kama wativyoshindwa mara kadhaa huko nyuma. Hata hivyo, kuna kitu watu wa aina hii wanakuwa hawajakifahamu bado ambacho ni kwamba kushindwa wakati mwingine ni fursa ya kujifunza na kupata uzoefu. Kwani makosa hutupa uzoefu na uzoefu hutupunguzia makosa. Kuna msemo mmoja wa kingereza naupenda sana ambao unasema failure teachs us the  way  by showing  us wich isn’t  the way. Yaani, makosa hutufundisha njia sahihi kwa kutuonyesha ipi siyo njia sahihi. Chukulia makosa kama fursa ya kujifunza na kusonga mbele vinginevyo utateseka na changamoto hiyo hiyo miaka nenda miaka rudi.

4.   Maneno waliyo wahi kuambiwa. Ndugu, moja ya kitu kina nguvu sana ni maneno hasa yanapo pandwa ndani ya moyo wako, haya yanaweza kuchukua mimba na kuzaa kitu kilicho pandwa kama ni chema watoto watakuwa ni wema sana na kama ni kibaya watoto watakuwa ni wabaya kulioko. Watu wengi wamekuwa wakitamkiwa maneno mengi hasi yaani, mabaya sana na watu wao wa karibu, watu kama , waalimu  wao, wazazi wao, wenza wao, ndugu zao na majirani zao  na maneno haya yamewavunja moyo kabisa kila wakitaka kusonga mbele ya kuendelea tena. Kitu hiki kimewafanya wawe ni watu wa kuanzisha vitu kwa muda na pindi wanapoyakumbuka maneno hayo mabaya waliyo wahi kuambiwa wanashindwa kabisa kuendelea mbele.

Ndugu yangu kanuni ya mwendelezo ukiivunja, utachelewa sana. watu utawachanganya na watakuona hueleweki maana kila muda unakuja na jambo hili na kuliacha lile, kitu hiki pekee kimewacost wengi sana . Ninajua kuna namna pengine ulikuwa ni mtu wa kughairisha mambo yako ya msingi. Na pengine umekuwa na mipango mingi sana, ndoto kubwa sana kitu hiki ni kizuri sana lakini hebu chagua kuanza na kitu kimoja kwanza kisha ukomae nacho hadi kieleweke, tafuta maarifa juu ya kitu hicho, jifunze kila siku na kifanye mara kwa mara na ikiwezekana ujitangaze utashangaa watu watakavyokua wanakupigia simu kwaajili ya kitu hicho yaweza kuwa labda ni  uandishi, kutengeneza sabuni, kulima, utaalamu wa kompyuta, uneni na mengine kede kede. Fanya kwa mwendelezo bila kuacha hata kama hujisikiii wewe fanya tu. Utashangaa watu tutakavyoaanza kukukuita professional , mtaalamu, professor, mkuu, boss, legend n.k. hapo ndipo utakapo kuwa umeanza kuukaribia ukuu unaoutafuta. Hata kama una mipango na malengo mengi tafuta kitu kimoja ambacho utaanza nacho kisha fanyia kazi, bila kuacha kisha anza kingine kama unao huo uwezo.

Labda nikuulize swali, je unataka kuwa mjasiriamali? Basi inakupasa ufanye ujasiriamali kwa mwendelezo. Je, unataka kuwa mwandishi bora? Anza kuandika kwa mwendelezo. Je unataka kuwa muhubiri maarufu? Anza kuhubiri kwa mwendelezo. Unataka kuwa mwigizaji bora? Igiza kwa mwendelezo. Je unataka kuwa mkulima bora? Lima kwa mwendelezo. Je unataka kuwa mfanyabiashara bora? Fanya biashara kwa mwendelezo. Je unataka kuwa mwalimu bora fundisha kwa mwendelezo. Mwendelezo! Mwendelezo! Mwendelezo! Nasema  mwendelezo, hiki kitu wazungu ndicho wanakiita consisitency. Hapa ndipo watu wengi hukwama na kupotea kabisa. Kama ulikuwa hujui hii, ni njia nzuri ya kujulikana na  maarufu, itumie sasa.

    Rafiki, ni matumaini yangu kuwa umejifunza kitu.

na kama unachangamoto katika hili pengine namna gani ya kuondokana na adha hii sasa waweza kuwasiliana na mimi moja kwa moja kupitia mawasiliano hapo chini naamini utasaidika.

GeT tO ThE nExT lEvEl!

Makala hii, imeandaliwa na kuandikwa na MIGONGO ELIAS Mshauri & Mwalimu Wa Saikolojia, Uchumi na Maisha. Mwanzilishi na Mwendeshaji wa Mtandao wa addvaluetz. Karibu sana ujiongezee thamani yako. 

Kwa mawasiliano;

Whatsapp & Sim >>+255767653697 /+255783327456

Email>> eliasmigongo120@gmail.com.

Facebook>> MIGONGO ELIAS.

LinkedIn>>Migongoe. 

Pinterest>>eliasmigongo.

Kama umejifunza kitu, niachie maoni yako nitafurahi kujifunza pamoja nawe

 

 

 

Popular posts from this blog

MAAJABU YA AKIBA

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 29

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 27.