MAAJABU YA AKIBA

Image
MAAJABU YA AKIBA Akiba (saving) ni kiasi cha fedha au rasilimali ambacho kimewekwa kwa matumizi ya baadaye, hata sasa kingeweza kutumika lakini umuhimu wake kwa kutumika baadaye ni mkubwa kuliko matumizi yake ya sasa. Hata katika biblia ``Mwanzo 41:35-36`` kama umewahi soma utaona Farao baada ya kutafsiriwa ndoto yake na kufahamu kuwa, imempasa kuweka akiba alilifanya hilo kwa uharaka ili kuhakikisha linaendelea vizuri ndio akamweka Yusufu kama msimamizi wa hili. Farao aliona kabisa kuwa nidhamu yake ya kujiwekea akiba haipo sawa hivo alihitaji msaidizi wa kumsaidia kama yeye alivyokuwa ndivyo tulivyo baadhi yetu siku za leo hatuwezi kujiwekea akiba ya vile tulivyo navyo. yaani huwa tunapenda kusema kesho itajisumbukia yenyewe,  Hata hivyo tangu zamani hata leo mataifa mbalimbali yamekuwa yakijiwekea akiba kwa manufaa na matumizi ya baadaye. Ukiangalia nabii Samweli alikuwa akijiwekea akiba na aliitoa pale Sauli alipomtembelea wakaila ile akiba ya chakula. Ni muhimu kujiw...

PANDE ZA MAFANIKIO

 


PANDE ZA MAFANIKIO


Mara nyingi MAFANIKIO huwa ni hitaji la Kila mtu.


Na hii huwa imebeba sehemu mbili muhimu.


1. SEHEMU YA KWANZA NI UPANDE WA MBELE( FRONT PART).


Sehemu hii huonyesha

 jambo hili kuwa ni zuri na ni jambo la kutamanika, kufurahiwa, na mengine kama hayo.


Huu unaonekana kwa macho ya nyama. Na watu hujua na kutoa sifa kemukemu.


Na huonekana  huleta hamasa, furaha, umaarufu, uhuru, heshima n.k


Siku zote watu waliofanikiwa na mafanikio yenyewe huonekana ni easy sana.


Na watu hulielezea Kwa urahisi naMSINGI WA NPGUVU YA MAFANIKIO. wa hali ya juu sana. 


Utasikia alienda secondary, akaenda chuo akawa bilionea, mara utasikia alianzisha biashara saivi ni mkurugenzi, alikuwa masikini akapewa mtaji saivi ni milionea.

Hapa mifano ni mingi sana.


2. SEHEMU YA PILI NI UPANDE WA NYUMA (BACK PART).


Upande huu mara nyingi hauonekani haraka.


Watu wengi husahau kabisa kuuangalia na kuusemea. Yaani chini ya kapeti namaanisha nyuma ya mafanikio...


Rafiki hii ni sehemu ya mchakato.


Ukiachana na raha na umuhimu wa mafanikio.


Huu ni upande wa kulipa gharama,  upande wa kufeli, upande wa mashaka, upande wa kujitoa mhanga, upande wa kukosolewa, upande wa kukataliwa, upande wa hali ngumu, upande wa kujitoa, upande wa kujenga nidhamu.


Kuyataja ni mengi sana, lakini nadhani umepata picha.


Na hii itukumbushe kuwa tunapotaka kufika sehemu ya kufanikiwa kwetu, kuna gharama na changamoto ambazo tutazipitia na lengo lake Si kutukatisha tamaa wala kutukomoa, bali ni kutuandaa ili kupata, kushukilia na kuhimili mafanikio tutakayo yapata.


Maandalizi yakiwa mabaya hii ni kusema kutokupata mafanikio au kupata na kushindwa kuhimili.


Na hii ni katika nyaja zote za maisha, kama ni michezo, kilimo, uandishi uongozi na mengine kama hayo.


Kinyume chake ni ukweli mtupu.


Upande huu ni chanzo, jikoni kunakopikwa mafanikio. Hapa ndipo mchakato wa mafanikio huandaliwa.


Ukifata mchakato na kuufanyia kazi, matokeo tarajiwa yatakuja tu.


Najua kunakitu umeongeza.

Mungu akusaidie sana.


Mwandishi>> Migongo Elias.

Mhariri >>> Erick Mgaya.


Ni matumaini yangu kuwa umejifunza kitu... Kama ndiyo waweza fanya yafuatayo.

1. Kama hujasave namba yangu waweza kusave Kisha unitumie jina lako WhatsApp nami nikusave uendelee kujifunza kila siku kupitia status.

2. Washirikishe wengine ujumbe huu wajifunze pia.

3. Unawezaa kutembelea ukurasa wetu wa Facebook Add Value Network. Au wasilina nami kwa masomo mengine ili kujifunza zaidi.

Let me sign out🖐️

MIGONGO ELIAS
Add Value Network
GeT tO tHe NeXt LeVeL 💪
eliasmigongo120@gmail.com
+255767653697

 

Comment (1)

Loading... Logging you in...
  • Logged in as
Ubarikiwe Saba Kwa ujumbe mzuri.

Post a new comment

Comments by

Popular posts from this blog

NJIA 7 ZA KUOSHA UBONGO WAKO.

VITU 9 MUHIMU KWA MTU YEYOTE KUJIFUNZA KWENYE MAHAFALI.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.