HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 26.

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 26. Ilipoishia.......... Alipomgeuza tu alishangaa kuona sura ya yule binti ni ya mbuzi. Aliogopa na kudondoka chini kwa kelele kuu alilia 'maaamaaaaaaa!!!!" Alijiokotaokota huku akiangukaanguka mpaka kwenye gari yake. Alipanda ndani ya gari na kuwasha gari. Alikimbiza gari mpaka akafika karibu na geti la nyumba ya Elvine, lakini kabla hajafika getini alishangaa kuona anaguswa mabegani ndani ya gari lake. Alitoa macho kwa uoga na mshtuko mkubwa mpaka akakosea njia na kwenda kugonga mti... Kusoma sehemu ya 25 bonyeza hapa. Sasa inaendelea......, Aligonga mti kwa nguvu mpaka naye akajipigiza kichwa kwenye usukani wa gari na gari ikaharibika sana upande wa mbele, alipona kwa neema tu kwa namna gari ilivyokuwa mwendo kasi angeweza hata kupoteza maisha lakini haikuwa hivyo. Alijikaza na kushuka kwenye gari akakimbia kuelekea kwenye nyumba ya Elvine,  njiani alikumbwa na kimbunga cha ajabu sana. Baada ya kile kimbunga kumpitia na kumzingazinga kwa muda

KATA TAMAA KUKATA TAMAA (GIVE UP TO GIVE UP)!

 

KATA TAMAA KUKATA TAMAA (GIVE UP TO GIVE UP)!

Kukata tamaa; Ni fikira  zinazo mfanya mtu kukosa tumaini la kusonga mbele au  kuendelea kufanya kile alicho jipangia kufanya, ili, kutimiza malengo yake. Fikira hizi humfanya mtu afikirie kuwa, changamoto alizo nazo ni kubwa kuliko uwezo alionao wa kukabiliana nazo. Ni hulka ya kila binadamu kupitia nyakati kama hizi za kukata tamaa. Hakuna binadamu asiye pitia kipindi hichi kwa baadhi ya nyakati. Nyakati kama furaha, huzuni, kukataliwa, kujichukia, kufeli, kudhalilika, kuheshimika, kudharaurika, kuwa maarufu, kupendwa, kuchukiwa, kutaka msaada, kutoa msaada, kukosea, kusamehewa n.k. Ni sehemu ya maisha ya kila binadamu kwa baadhi ya nyakati. Nyakati kama hizi ndizo huleta radha ya maisha. Vinginevyo maisha yangekosa radha kabisa. Na watu kwa kushindwa kulitambua hili wamejikuta wakikata tamaa na kushindwa kuendelea tena kwa yale waliyo jiwekea.

Zipo sababu zinazo wafanya watu wengi kukata tamaa na kushindwa kusonga mbele katika kufanikisha mipango yao  waliyo jiwekea ambazo ni;

1.   CHANGAMOTO WANAZOKUTANA NAZO;

Pamoja na kwamba changamoto ni sehemu ya maisha, watu wengi wanashindwa kukubaliana na jambo hili. Ndiyo maana wamekuwa wakikata tamaa kila wanapo kutana na changamoto. Jifunze hili na tambua kuwa changamoto zinapo kuja kwako,  zinakuja na somo au fundisho fulani kwako. Lijue funzo hilo ili uweze kufaidika na kila changamoto unayo kutana nayo. Afu by the way, kukata tamaa ni dhambi ujue!

 Thomas Packet Mfanya biashara maarufu nchini mareka. Alifanya kazi kwa kujituma hadi kufikia umri wa miaka 50 alikuwa  Bilionea tayari. Siku moja mfanya kazi wake mmoja alikutwa amekufa ofisini kwake. Uchunguzi ulifanyika na iligundulika kuwa yeye ndiye aliye fanya mauaji hayo. Kesi ikafika mahakamani, alitumia takribani pesa zake zote bila mafanikio hadi kufilisika. Hivyo mahakama ikaamru Thomas afungwe kifungo cha maisha kwa kosa la mauaji hayo. 

 Baada ya miaka kadhaa kupita, ikaja kugundulika kuwa Thom hakuhusika na kile kifo. Hivyo aliaachiliwa huru na kurudi tena mtaani. Thom alikuwa na afya mbovu sana, umri ulikuwa umeenda na alikuwa tayari kashafilisika. Pia alikuwa hana sehemu ya kwenda alikuwa analala mtaani katika gereji moja ya aliyekuwa rafiki yake katika maeneo ya Washngton Marekani. Marafiki na watu wengine walimcheka sana kwa kufilisika kwake.

Maisha ya Thom hayakuwa si mazuri hata kidogo. Kutokana na changamoto hizo  hakuona thamani ya kuishi tena. Alikosa maana ya kuishi kwake na hivyo alikata tamaa na kuamua kujiua kwa kunywa vidonge 35 vya usingizi.

 Baada ya muda alikuja kuzinduka akajikuta yupo hoi, hospitali kwa kusaidiwa na wasamalia wema.

Thom alisema alipokuwa karibu na kukata roho, alisikia sauti ikimwijia na kumwambia mambo mawili ambayo ni,

a)    Maisha yako ni wajibu wako wewe mwenyewe 100%, hivyo unauwezo wa kuyajenga au kuyabomoa.

b)   Mali na fedha ambazo ulizipata hukuja nazo. Kuna mambo ulifanya na kuzipata, hata sasa unaweza kufanya mambo hayo  na ukapata tena zaidi ya mwanzo. Huna sababu ya kukata tamaa. 

Kuanzia hapo Thom hakuwa na tabia ya kutaka kukata tamaa tena. Aliamua kwenda kufanya kazi kwa bidii na maarifa na baada ya Muda kupita alirudi tena katika utajiri wake na alikuwa mtu tajiri zaidi ya alivyokuwa awali. 

Kuna mambo mengi sana ya kujifunza kutoka kwa huyu jamaa, yaani, pamoja na umri kwenda, kupoteza mali na utajiri wote aliokuwa nao, kusingiziwa kesi ya mauaji, kukataliwa na watu, magonjwa na mengine mengi. Changamoto hizi kwakweli hata wewe msomaji zingekupata sijui ingekuwaje...

Lakini tunaona kwa Bwana Packet ilikuwa tofauti kabisa, alipata Nguvu na kuendelea mbele tena, kubwa zaidi akapata kile alicho kitaka tena alipata  zaidi. Hivi packet angekata tamaa ingekuwaje? Nadhani asingetimiza ndoto yake kabisa. Hivyo usikubali kukata tamaa kizembe pambania ndoto yako. Tambua changamoto ni sehemu tu ya maisha na  haziji kukuumiza wala kukukomoa bali zinakuja kukupa somo jifunze usonge mbele.

kujifunza zaidi namna ya kukabiliana na tatizo lolote bonyeza hapa

2.   MANENO HASI WALIYOWAHI KUAMBIWA;

Wapo watu wengi sana wamerudi nyuma na kukata tamaa kutokana na maneno waliyo wahi kuambiwa. Maneno haya mara nyingi huwa ni Maneno hasi na yanakatisha tamaa kwelikweli. Nunaweza ukawa umeambiwa na watu wako wa karibu sana. Mfano waalimu, ndugu, mwenza wako, majirana n.k.

Na watu hawa wanaweza wakawa walisha fanya jambo hilo na  wakashindwa, hivyo kila ukitaka kujaribu kufanya wanamwambia haiwezekani. Mara nyingi lengo lao huwa wanataka kukusaidia ili usipate hasara kama wao walivyo pata hasara. Hapa kumbuka kabla hujapokea ushauri wa namna hii usikubali kwa maana kila mtu anauwezo tofauti na wengine lakini pia, “watu hatufanani na hatuwezi kufanana”.

Lakini wapo watu ambao wao huwa wameshindwa katika eneo hilo na hawataki mtu mwingine afanikiwe kwani atawadhalilisha. Hivyo kila utakapo jaribu watakwambia haiwezekani yaani, hawataki washindwe peke yao, watakwambia maneno hasi ili na wewe ukate tamaa.

Watu wengine ni wale watu wenye wivu wa kijinga  ambao wanawaonea wenzao gere, katika kusonga mbele, hawataki wengine wafanikiwe kama wao walivyofanikiwa watawakatisha tamaa sana.

Kuwa makini na wakatisha tamaa wa namna yeyote ile, iwe ni wazazi, waalimu, rafiki, majirani n.k. Kataa kukata tamaa hadi mkatisha tamaa akate tamaa. Kataa kisha jiamini mwenyewe, jitamkie maneno chanya na kataa maneno hasi kwenye maisha yako. Hivi unafahamu kuwa kila neno moja hasi ukitamkiwa linahitaji maneno 17 chanya ili kuliondoa? 

3. HITILAFU YA MIILI AU MAUMBILE YAO;

Nakosa namna nzuri ya kuiweka pointi hii, lakini nina uhakika utanipata vizuri tu. Kuna watu kutokana na maumbile yao, hitilafu walizo nazo aidha ni kwa kuzaliwa au kwa kupata ukubwani katika maisha yao. Kitu hiki kimekuwa ni kikwazo kikubwa na kisingizio lukuki cha watu wengi hata kukata tamaa katika kutimiza malengo yao.

 Hivi unamfahamu mwana dada mmoja anayeitwa Haben Girma wa Marekani? Amezaliwa na tatizo la kutokuona (blind) pamoja na kutokusikia (deaf). Haben tangu akiwa mtoto alikuwa na ndoto ya kuwa mwanasheria mkubwa sana kuwahi kutokea. Ana wadogo zake ambao nao wanatatizo kama lake mama yake alikuwa mkimbizi kutoka nchini Eritiria na anaishi marekani kama mkimbizi.

Haben pamoja na kuwa na ndoto kubwa ya kuwa mwanasheria. Lakini akiiangalia familia yake hamna wa kumtegemea wadogo zake ndiyo hivyo tena. Kuna wakati ulifika hadi akakata tamaa kama binadamu lakini, baada ya kutafakari sana kuhusu ndoto yake  hakujali tena juu ya hali aliyokuwa nayo. Aliamua kupambana na hakutaka kuonewa huruma na mtu na aliamua kupambana ili kutimiza ndoto yake ya kuwa mwanasheria. Alifanikiwa kuwa mwanasheria wa kwanza wa aina hiyo kuhitimu katika chuo kikuu cha Havard nchini Marekani. Na alitimiza lengo lake la kuwa mwanasheria.

 Ndugu kama mlemavu huyu hakukata tamaa na ametimiza lengo lake, wewe mtu uliye mzima kabisa si zaidi ?

Usije kukata tamaa kwa sababu ya maumbile na mwonekano wa mwili wako. Pambania Ndoto zako, uzitimize. Halafu, kukata tamaa hakutatui tatizo ujue!

 Katika hili nina mifano mingi sana ya kukuambia. Hivi unampata Nick Juviccic ambaye, alizaliwa Tarehe 04.12.1982 Australia. Akiwa hana miguu wala mikono. Alipitia changamoto nyigi sana kama vile, kukata tamaa, msongo wa mawazo na nyingine kibao. Lakini alijifunza kuzishinda, kutokukata tamaa na kuendana nazo, akafanikiwa na alianza kutoa hamasa aikiwa na umri wa miaka 19, Mwinjilisti, Mwandishi wa vitabu, mfano  wa kitabu alichoandika ni life without limits, ana mke na watoto wanne, mwanzilishi na mkurugenzi mtendaji wa kampuni isiyo ya kiserikali ya watu wasio na miguu wala mikono duniani. Pia, ni mwana hamasa na amesafiri nchi nyingi sana duniani kutoa hamasa na kuwatia moyo watu. Kama unabisha kamuulize google.

Daah! Naandika huku nikisikitika sana, wakati mwingine Mungu mwacheni aitwe Mungu tu jamani, hivi haya si ni maajabu kabisa asee! yaani, mtu hana miguu wala mikono eti anahangaika kumtia moyo mtu ambaye ana mikono na miguu yote, ambaye pengine tu alisumbuliwa na mafua, miguu kuwaka moto, kichomi, njaa, kukataliwa na wazazi, kuumwa, kufeli mtihani, kukosa mtaji n.k. 

Katika hili nimejifunza kuwa, nguvu ana uwezo wa mtu upo ndani yake, yaani,  mtu halisi ni yule wa ndani na siyo hii miili na maumbile yetu ya nje. Haya ni sawa na nyumba tu ya utu wetu wa ndani. Sababu tumeona watu wenye mionekano isiyo waruhusu kuendelea lakini, hawakutaka kukata tamaa na kuwa omba omba kama wengine wanavyofanya. Sikatai kuombaomba lakini, hili nalo la kukata tamaa tuliangalie kwa jicho la tatu.Vinginevyo, tuache masihara na kama ulifikiria kukata tamaa fikiri tena.

4.   KUSHINDWA MARA KWA MARA;

Mtu kama Thomas Edson karibuni kila mtu anaelewa habari zake ambaye hadi sasa tunanufaika na ugunduzi wake wa taa (bulb). Gwiji huyu alifanya majaribio ya kutengeneza taa mara 999 bila, kukata tamaa na raundi ya 1000 alifanikiwa kutengeneza taa ambazo tunatumia hadi leo hii.

 Lakini kikubwa sana katika hili napenda alivyo jibu baada ya kuuliza kuwa, kwanini ulishindwa mara 999? Alijibu na kusema sikushindwa mara 999, ila nilijifunza njia 999 za kutokutengeneza taa kwa usahihi.

Mtu huyu alichukulia kushindwa kwa faida na si kulalamika na kukata tamaa kama baadhi ya watu wa sasa.

Mtu mmoja akauliza nishindwe mara ngapi ili nikate tamaa? Hivi mtu kama huyu wewe ungemjibuje? Rafiki! Ukiona umeshindwa siku moja acha utani endelea kufanya kazi, mara kumi acha utani endelea kufanya kazi, wiki moja acha utani endelea kufanya kazi, mwaka mmoja acha utani na sema endelea kufanya kazi hadi kieleweke. Haijalishi utashindwa mara ngapi, rudi kapambane hadi kieleweke labda kama siyo ndoto yako na hauipendi kabisa. Vinginevyo acha utani piga kazi.

 Wakati mwingine tutaangalia namna ya kufanya unapo hisi kukata tamaa!

 

Rafiki! ni matumaini yangu kuwa umejifunza kitu.

na kama unachangamoto katika hili pengine namna gani ya kuondokana na adha hii wasiliana na mimi moja kwa moja kupitia mawasiliano hapo chini naamini utasaidika.

GeT tO ThE nExT lEvEl!

Makala hii imeandaliwa na kuandikwa na MIGONGO ELIAS Mshauri & Mwalimu Wa Saikolojia, Uchumi na Maisha. Mwanzilishi na Mwendeshaji wa Mtandao wa addvaluetz. Karibu sana ujiongezee thamani yako. 

Kwa mawasiliano;

Whatsapp & Sim >>+255767653697 /+255783327456

Email>> eliasmigongo120@gmail.com.

Facebook>> MIGONGO ELIAS.

LinkedIn>>Migongoe. 

Pinterest>>eliasmigongo.

Kama umejifunza kitu,niachie maoni yako nitafurahi kujifunza pamoja nawe  

 

 

Popular posts from this blog

GHARAMA 5 ZA KUUFIKIA UKUU UNAOUTAKA.

USIKUBALI KUAJIRIWA KABLA HUJASOMA HAPA.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.