HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 26.

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 26. Ilipoishia.......... Alipomgeuza tu alishangaa kuona sura ya yule binti ni ya mbuzi. Aliogopa na kudondoka chini kwa kelele kuu alilia 'maaamaaaaaaa!!!!" Alijiokotaokota huku akiangukaanguka mpaka kwenye gari yake. Alipanda ndani ya gari na kuwasha gari. Alikimbiza gari mpaka akafika karibu na geti la nyumba ya Elvine, lakini kabla hajafika getini alishangaa kuona anaguswa mabegani ndani ya gari lake. Alitoa macho kwa uoga na mshtuko mkubwa mpaka akakosea njia na kwenda kugonga mti... Kusoma sehemu ya 25 bonyeza hapa. Sasa inaendelea......, Aligonga mti kwa nguvu mpaka naye akajipigiza kichwa kwenye usukani wa gari na gari ikaharibika sana upande wa mbele, alipona kwa neema tu kwa namna gari ilivyokuwa mwendo kasi angeweza hata kupoteza maisha lakini haikuwa hivyo. Alijikaza na kushuka kwenye gari akakimbia kuelekea kwenye nyumba ya Elvine,  njiani alikumbwa na kimbunga cha ajabu sana. Baada ya kile kimbunga kumpitia na kumzingazinga kwa muda

MAMBO 6 YANAYOPUNGUZA THAMANI YAKO.

MAMBO 6 YANAYOPUNGUZA THAMANI YAKO.

Hivi ulishawahi kuona aina hizi mbili za watu? 1.watu ambao wanaheshimika na kuthaminiwa sana katika jamii. Yaani, hawa watu kwenye masuala muhimu yanayo hitaji ushauri, uamuzi, na mchango wowote wenye tija ni lazima wahusishwe katika kufanya hivyo. Iwe katika vikao na matukio mengine muhimu hapo utasikia wakisema kamwiteni fulani, mwandikieni barua fulani au mpigieni simu fulani atasaidia sana katika hili.

2. Upande mwingine Kuna watu ambao huwa wanapuuzwa sana na kuonekana hawana mchango wowote katika jamii, watu hawa ni ngumu sana kukuta wemeombwa hata ushauri au kushirikishwa kwenye masuala muhimu katika jamii. Utasikia tu hamuna chochote hapo, mtapoteza hela bure tu.Watu hawa wanapuuzwa na kuchukuliwa poa sana pengine kutokana na matendo yao, manrno yao, tabia na mionekano yao katika jamii. Zipo sababu nyingi zinazofanya mtu kupuuzwa na kuonekana wa kawaida sana, hizi tutaziangalia wakati mwingine.

Lakini leo nataka tuangalie mambo ya yanayosababisha thamani ya mtu kupungua katika jamii anayoishi. Hapa chini ni mambo yanayoshusha thamani yako katika jamii yako ambayo ni;

1.   KULALAMIKA (LAMENTING).

Tabia hii ya kulalamika si nzuri hata kidogo, kuna watu ni wazuri wa kulalamika, huwa wanalalamika hata kama kitu ni kidogo sana kimemtokea atalalamika usiku na mchana. Iwe ni tatizo limemkuta atalalamika kweli kweli. Watu wa aina hii wakikutana na changamoto kidogo tu utasikia kwanini mimi linipate hili, kwanini Mungu nilizaliwa Tanzania? Yaani, ni full kulalamika na unakuta mtu anamlalamikia hadi Mungu hivi ni kweli jamani. Kwa lugha fupi mtu huyu anawaombea watu wengine wapate mabaya. Ndugu yangu changamoto zitakuja tu hata kama uwe mwema au muovu kiasi gani zitakuja kwako na kama hautakuwa tayari kuzikubali na kuzikabili utapata tabu sana,lakini pia nikwambia changamoto inapokuja inatabia ya kukufundisha na kukuimarisha, hivyo jitahidi kupata funzo kwa changamoto yako ili uimarike kuliko kulalamika sana. Rafiki tabia hii ukiendekea nayo watu watakudharau sana na thamani yako itashuka kabisa. Hapa badala ya kulalamika uwe ni mtu wa leta suluhu katika changamoto zako na watu wenginebkuliko kulalamika muda wote.

2.   KUOMBA OMBA (DEMANDS).

Nakubali kwamba hakuna binadamu aliyekamilika hayupo. Ndiyo maana katika dunia hii tunaishi kwa kutegemeana hivyo kutoa na kuomba ni swala la kawaida kabisa. Lakini unapokuwa mtu wa kuomba omba kila wakati na kwa kila mtu utashusha thamani yako mapema sana. Omba kwa utaratibu na heshima tena kwa watu unao dhani kuwa watakusaidia na siyo kuonba kwa kila mtu. Ulisha wahi kuona mtu kila ukikutana naye au kupiga simu au kuona sms yake anaonba yaani, unajua kabisa kwamba hii simu siyo bure na kweli ukipokea utasikia boss nipe teni nimekwama hapa mkuu tena bila hata kuomba kama ni yake vile, au mwingine anakwambia boss niazime 60000 kesho kutwa narudisha mapema sana, kesho kutwa yenyewe sasa ikifika. Rafiki unapokuwa na uhitaji tafuta msaada lakini isiwe ndiyo tabia yako wakati mwingine wasaidie na wengine usiwe ni mtu wa kuomba tu.Badala ya kuomba omba uwe mtoaji mzuri pia.

3.   VISINGIZIO (EXCUSES).

kunamsemo unasema mbaazi akikosa maua husingizia jua. Watu hawa huwa wanasababu katika kila kufeli kwao na wanazifanya kuwa halali kabisa, ukimwambia kwanini hujalima mwaka huu atakwambia mvua haikunyesha, kwanini hukumaliza kazi atakwambia nilipata imejensi, kwanini hukuja kwenye kikao atakwambia nilikuwa nafua na wakati huo mtu anafahamu kabisa kuwa wakati fulani anatakiwa awepo kwa kikao au afanye kazi fulani lakini inakuwa tatizo. Hii inatokana na uwezo mdogo wa kusema hapana. Rafiki badilika acha visingizio kama mbaazi wakosavyo maua na kusingizia jua isiwe kwako asee piga kazi achana na excuses na kama kitu huna uwezo nacho wa kukifanya mwambie mtu ukweli kwa kusema hapana kwa heshima kuliko kukubali ili kumridhisha kisha baadaye ukaleta visingizio vya kutosha kumbe hata kitu hicho ulikuwa hukiwezi asee. Sasa badala ya kuwa na visingizio viepuke kwa kuanza kufanya na kuendelea kufanya mpaka kieleweke.

4.   SIFA NA MAJIVUNO.

Tabia hii pia si nzuri sana hasa kwa jamii inayo kuzunguka, lakini imekuwa ni hulka ya watu wengi kupenda kujisifia au kusifiwa kwa maendeleo yao, tabia zao, hatua wanazo zipiga. Ukweli ni kwamba hakuna mtu ambaye hapendi kusifiwa hayupo sijaona kwakweli, lakini kuna watu wamezidi sana kutaka sifa, utashangaa mtu kupiga hatua na kufanikiwa kidogo tu mtaa mzima watajua, akipata pesa kidogo tu watu wote watajua, akiongea kingereza kidogo tu mtaani watajua, yaani, ni full kutamba na kujivuna. Ajabu kubwa ni kwamba mtu huyo huyo aliyekuwa anajivuna utashangaa jioni anakuomba pesa akamwagilie moyo. Ukimuuliza imekuwaje tena, anakwambia ni lazima watu wajue kuwa unazo hata kama unapumulia mpira. Nikaja gundua kumbe watu hawaishi uhalisia wa maisha yao badala yake wanaishi ili kuwaridhisha watu wengine tu. Hii nayo ni hatari na itashusha thamani yako.

Ndugu yangu kama kuna kitu kizuri umekifanya wacha watu waseme wenyewe na mambo yatakaa vizuri tu. kuliko kuanza kujisifia mwenyewe kufanya hivyo ni kupoteza muda kama walivyo sema wataalamu kuwa “Be a better person but don’t waste time to prove it”. Kuwa mtu bora lakini usipoteze muda kuthibitisha asee.

5.   UONGO NA KUKOSA UAMINIFU.

Kuna watu uongo wameufanya kuwa ni sehemu ya maisha yao. Yaani, wanaongea ongea tu bila hata kufikiria, wanatoa ahadi ambazo si halisi katika maisha yao na matokeo yake wanashindwa kuzitimiza na wanakuwa waomgo, hivyo kuvunja uaminifu. Ndugu uaminifu ni kutunza na kusimamia maneno yako. Kushindwa kufanya hivyo unakuwa  muongo na unakosa uaminifu. Tambua kuwa “truth and loyalty are the best policies” yaani ukweli na uaminifu ni sera bora sana. Pia kuna msemo mmoja mzuri sana unasema “When  you don’t keep your words you lose credibility, when you lose credibility, you break the bond of trust. And breaking the bond of trust ultimately leads to a string of broken relationships” tafisiri yake ni kwamba ukishindwa kutunza maneno yako unapoteza uaminifu wako na ukipoteza uaminifu una vunja uaminifu . Na kuvunja uaminifu hupelekea mahusiano kuvunjika.

kujua zaidi kuhusu ukweli na uaminifu bonyeza hapa

6.   KUWAPUUZA NA KUTOKUWASIKILIZA WENGINE.

Hiki ni kitu kidogo sana ukikifanya lakini madhara yake ni makubwa mno . Watu wengi wamekuwa wakiwapuuza na kutokuwasikiliza kabisa wengine, mara nyingi wamekuwa ni watu wa kutaka kujaliwa na kusikilizwa wao tu. Hiki kitu ni ngumu kutokea hata kikitokea ujue wanakunafikia tu ukiondoka watakusema kweli kweli na kukuita majina yote yatakayokufaa. Kubwa kabisa hapa jifunze kuwajali watu wengine, jifunze kusikiliza watu tena kwa makini, utapata faida mara mbili ya utakavyoongea. Sikiliza na kuwajali wengine hasa wanapohitaji msaada wako, ukitaka kusikilizwa wasikilize kwanza watu wengine, ukitaka kuheshimiwa waheshimu kwanza watu wengine, ukitaka kuthaminiwa wathamini kwanza watu wengine. Kwani, “what goes around comes around”.

 

Rafiki! ni matumaini yangu kuwa umejifunza kitu.

Na kama unachangamoto katika hili pengine namna gani ya kuondokana na adha hii wasiliana na mimi moja kwa moja kupitia mawasiliano hapo chini naamini utasaidika.

GeT tO ThE nExT lEvEl!

Makala hii imeandaliwa na kuandikwa na MIGONGO ELIAS Mshauri & Mwalimu Wa Saikolojia, Uchumi na Maisha.  Mwanzilishi na Mwendeshaji wa mtandao wa addvaluetz  karibu sana ujiongezee thamani yako. 

Kwa mawasiliano;

Whatsapp & Sim >>+255767653697 /+255783327456

Email>> eliasmigongo120@gmail.com.

Facebook>> MIGONGO ELIAS.

LinkedIn>>Migongoe. 

Pinterest>>eliasmigongo.

Kama umejifunza kitu,niachie maoni yako nitafurahi kujifunza pamoja nawe.  

 

Popular posts from this blog

GHARAMA 5 ZA KUUFIKIA UKUU UNAOUTAKA.

USIKUBALI KUAJIRIWA KABLA HUJASOMA HAPA.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.