Posts

Showing posts from June, 2023

HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 31

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 31 Ilipoishia………. Elvine alipoteza amani kuliko hata mkewe maana kila alipomtazama mkewe basi moyo wake ni kama ulikuwa unachomwa na mwiba uliojishikiza huko kwenye mishipa ya moyo. Nafsi yake ilitaabika na ndipo alipoamua kutafuta muda mzuri, baada ya chakula cha jioni, azungumze na mkewe, maana ule ukimya wa siku mbili ulikuwa adhabu kubwa sana kwake. Kusoma sehemu ya 30 bonyeza hapa Sasa inaendelea………. Elimina mamy naomba kujua kwanini hutaki kuniuliza kuhusu sababu ya haya yote? Maana najua unajua kuwa kuna mahali mimi nilikosea, sasa unapokaa kimya hivyo… kiukweli unazidi kunichanganya maana ni kama hutaki kujua, sasa unadhani mimi roho yangu itatulia kweli?. Hata kama ungekuwa wewe lazima usingepata amani, ungekuwa hata unawaza hivi nakuwaziaje, nakuonaje na ninajisikiaje ninapokuona, sasa kwanini wewe umekaa kimya, sema neno tafadhali? (Elvine alikuwa akiongea bila kumtazama mkewe usoni maana moyo wake haukuwa katika hali ya utulivu). Pamoja na ...

SIMULIZI YA KUSISIMUA KUHUSU “HATIMA YA KIMUNGU”. >>SEHEMU YA TATU.

Image
  SIMULIZI YA KUSISIMUA KUHUSU “HATIMA YA KIMUNGU”. >>SEHEMU YA TATU.   Ilipoishia....,.. Editrin baada ya kutulia alimsimulia kisa kizima mama yake tangu alipotoroka kwao, hadi kufikia hapa alipo na namna amba v yo El vine alivyopotea. Eliana alionesha kuumia sana kwani kwa namna nyingine tunaweza kusema yeye ndi y e aliyekuwa bibi wa mtoto yule. Wakiwa wanaendelea na mazung u mzo y ale Editrin akaanza kukumbuka kisa chote kilichomkuta kwenye maisha yake hata kupelekea yeye kutoroka kwao Dar es salaam na kuamua kuja kuishi Iringa.......   Kama hujasoma sehemu ya kwanza na ya pili bonyeza hapa. Sasa inaendelea...,.... Editrin alizaliwa Katika familia ya kitajiri sana. Baba yake alikuwa akiitwa Mr. Edward na mama yake aliitwa Eliana . Katika familia yao walizaliwa watoto wawili tu! ambao ni Editrin na Edger. T angu utoto wao walipendwa sana na wazazi wao wote wawili. Editrin na k aka yake Edger hawakuwahi kuyajua maisha ya shida ma an a baba yako ali...

JIFUNZE KUJIFUNZA (PART 1)

Image
JIFUNZE KUJIFUNZA (PART 1) Siku moja nikawa nimetulia natafakari   nikawaza na kuwazua kuhusu binadamu. Nikaona kuwa ni kawaida kabisa kwa binadamu yeyote kuzaliwa, kulelewa, kwenda shule au kutokwenda kabisa, kuoa/kuolewa wakati mwingine kutokuoa/kuolewa kabisa, kufanya kazi, kuzeeka na hata kufa. Lakini unaweza kufa hata kabla ya wakati wa kuzeeka kwako. Nikagundua kuwa katikati ya utoto na uzee/ kifo. Mwanadamu huyu atajikuta amefahamu vitu vingi sana. Aidha kwa kujifunza mwenyewe kwa kuona kusikia au kwa njia yeyote ile, au kwa kufundishwa na watu wengine nyumbani au kwa kwenda shule. Kwa kifupi   tumejifunza au tumefundishwa mambo kemkemu. Ukienda shule za St. Kayumba utafundishwa habari ya 3K   yaani, kusoma, kuandika, na kuhesabu. Na, ukibahatika ukapanda magari ya njano utafundishwa kuhusu, 3R s yaani, Reading, wRiting, and aRithmetic. Hata kwa wale hawakukanyaga kabisa umande wa asubuhi nao wamejikuta wamejifunza vitu vingi sana huko nyumbani na mtaani pia. ...

Popular posts from this blog

MAAJABU YA AKIBA

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 29

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 27.