Posts

Showing posts from September, 2023

USISAHAU KILICHOKULETA HAPO.

Image
  USISAHAU KILICHOKULETA  HAPO. Kuna makosa mawili makubwa ambayo watu wengi hufanya wanapoanza kuyaona mafanikio yao: wanasahau walikotoka, na wanasahau kilichowafikisha hapo. Haya ni makosa makubwa mawili, ni kesi ya kutokujitambua. Hapo ndipo safari yao huanza kushuka bila wao kujua yaani, kimya kimya. UKWELI AMBAO NIWACHACHE WANAUJUA, Mafanikio hayakuji kwako kwa bahati mbaya. Yalikuja kwa sababu ya vitu fulani ulivyofanya. Yamkini huenda; Ulijituma sana, Ulijinyima, Ulijifunza, Uliomba sana, ulisave sana, Ulijitoa zaidi kuliko wengine, Ulivumilia wakati mgumu. 👉 Hiyo ndiyo “formula” yako ya mafanikio. Lakini shida inaanza pale unapopata mafanikio walau kidogo, halafu ghafula unaanza kubadilika. UNAPOSAHAU KILICHOKULIPA, UNAPOTEZA MWELEKEO WAKO. Watu wengi wakianza kuona matokeo: Wanaacha nidhamu, Wanaacha kujifunza, Wanaanza kujiamini kupita kiasi, Wanasahau kujituma, Wanaanza maisha ya anasa mapema sana. Kisa wameona matokeo kidogo tu. Namatokeo yake,...

SIMULIZI YA KUFURAHISHA, “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”. SEHEMU YA KUMI NA TANO.

Image
SIMULIZI YA KUFURAHISHA, “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”.   SEHEMU YA KUMI NA TANO.  Ilipoishia... Usisogee maana hapo unaposogea ndipo nataka kudondokea kwahiyo pishaaa!!" Kabla hajayatafakari yale maneno yule mtu alijiachia makusudi kabisa na kujitupa chini. Elvine alishangaa zaidi. Alitaka kusogea ili akatoe msaada lakini yule mtu ghafla alipotea.         Elvine alipata hofu zaidi. Akakimbia mpaka chumbani kwake na akajihisi kabisa hadi ile kiu imekata. Lakini alipofika chumbani kwake alipigwa na butwaa kwa kile alichokuwa anakiona mbele yake na wala hakuamini kwa haraka.... Kusoma sehemu ya 14 bonyeza hapa Inaendelea...     Alipotazama kitandani kwake alimuona kijana yule aliyekuwa kaanguka mchana na ndiye aliyemuona kajiangusha muda sio mrefu kutoka kwenye ngazi tena akiwa anacheka sana.       "Kumbe ni wewe? Unajua nilikuwa najiuliza sana kuwa ni kijana yupi ambaye anakaa hapa na anauwezo wa kufanya mambo makubwa. Kwakwel...

SIMULIZI YA KUFURAHISHA, “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”. SEHEMU YA KUMI NA TATU.

Image
  SIMULIZI YA KUFURAHISHA,   “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”. SEHEMU YA KUMI NA TATU.     Ilipoishia..   Aligundua kuwa kumbe Elimina anamachungu sana moyoni mwake. Aliacha kumfokea na kuanza kumwomba msamaha huku akitamani kujua tatizo ni nini hasa. Wakati akiwa anambembeleza alikaa pembeni ya Elimina kwenye sofa huku akisema samahani. Ghafla mama aliingia na kushangaa kwa kile alichokiona "Nyie watoto ni upuuzi gani mnafanya hapo?....." kusoma sehemu ya kumi na mbili bofya hapa   Sasa inaendelea....   Elvine hawakujua wamjibi nini maana walijua kabisa mama atakuwa kaelewa kwa tofauti sana.     "Samahani mama sio kama unavyofikiria. Ni kwamba Elimina hajisikii vizuri. Na alikuwa akilia na mimi sijui shida ni nini na ndio maana nilitaka aniambie" Elvine alijaribu kujitetea       "Jiandaeni kwaajili ya kikao cha familia akija baba yenu" mama aliongea kwa mkato kisha akaondoka na kuelekea chumbani. ...

Popular posts from this blog

UKIJUA HILI KUHUSU WATU UTAFANIKIWA SANA.

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 29

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 27.