Posts

Showing posts from March, 2024

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 29

Image
  Nashukuru kwa kushiriki nami link ya Hadithi hii tamu na Nzuri ya Hatima ya Kimungu Sehemu ya 29. 🙏 Nilichosoma katika sehemu hii, simulizi imeendelea  kwa mvuto mkubwa sana – linaonyesha mapambano ya ndani ya Elvine kati ya imani yake, hofu yakuwaza kumpoteza mkewe Elimina, na hatia ya makosa ya zamani. Kuna mambo yafuatayo nimeona  yaliyobeba msingi   wa  sehemu hii: 1. Mgongano wa nafsi ya Elvine 👉Anapokuwa mbele ya Malaika Elvila, anatakiwa kufanya maamuzi magumu: kati ya mke na mtoto. 👉Uamuzi wake unaonyesha upungufu wa mwanadamu, uchungu, na jinsi maumivu yanavyoweza kuathiri fikra na maamuzi. 2. Adhabu na Neema 👉Kupotea kwa mtoto na kutozaa tena kwa Elimina ni matokeo ya makosa ya Elvine, lakini bado neema ya Mungu inaonekana kwa kumrejesha mkewe. 👉Malaika anamkumbusha kuwa Mungu si mkatili, bali anamfundisha kupitia mateso na changamoto. 3. Ugeuzi wa Maisha (Turning Point) 👉Elvine sasa anaitwa kuwa mchungaji wa kondoo wa Bwana, ishara ...

SIMULIZI YA KUFURAHISHA, “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”. SEHEMU YA 17.

Image
HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA KUMI NA SABA Ilipoishia.... Siku moja akiwa amelala aliota moto mkubwa unawaka ndani ya maji lakini ule moto ni kama unaofifia kwa kuzidiwa na yale maji. Alipoamka akaikumbuka ndoto aliyowahi kuota utotoni ikamkumbusha kuwa hatakiwi kuzima namna hiyo na akajikuta kakumbuka sana vile viusumbufu vya kivita na maadui. Lakini hakujua kumbe kuna bomu kubwa kaandaliwa.....  Kusoma sehemu ya 16 bonyeza hapa. *.   *.    *.   *.    *.    *.   *.  Elvine alikuwa ameketi juu ya mti katikati ya poli fulani akiwa na amani sana. Akiwa pale aliweza kuona umbali mrefu sana. Alishangaa baada ya kumuona mtoto wa kiume mwenye umri kama wa miaka 7 hivi anazunguka zunguka mule polini. Akacheka sana halafu akasema "Kuna vitoto vya ajabu Duniani jamani. Sasa angalia huyu mtoto anataka nini huku polini muda huu?" Akatabasamu akachuma embe lililoiva kwenye ule mti na kuanza kulila. Yule  mtoto alikuwa akijiimb...

SIMULIZI YA KUFURAHISHA, “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”. SEHEMU YA 16.

Image
  SIMULIZI YA KUFURAHISHA, “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”.   SEHEMU YA 16.  Ilipoishia.....      Sherehe zilianza na watu wengi sana walikuja tena wachungaji walikuwa wengi sana. Elvine alifurahi baada ya kumuona baba yake na mama yake wamekuja tena wakiwa wazima wa afya. Elvine pamoja na kufurahi lakini bado alikuwa na wasiwasi  k usoma sehemu iliyopita bonyeza hapa. Sasa inaendelea.... Alitazama Elimina namna alivyopenda akasema kimoyomoyo 'hakika malkia wangu usife mapema bado natamani kuona ulipendeza hivihivi daima'. Wakaingia kanisani ambapo aliyesimamia ibada ya send-off alikuwa ni mchungaji wa kanisa jilani. Lakini Elvine alikuwa na wasiwasi sana na yule mchungaji maana tangu alipofika alikuwa hawatazami watu usoni bali mda mwingi alitazama chini kama anayetunza sheria za familia.  Elvine hakutaka kujaji saana lakini kuna namna alimkazia macho sana yule mchungaji maana kwa mauzauza tu yanayomuwinda aliona ni lazima amchunguze kila mtu ana...

Popular posts from this blog

MAAJABU YA AKIBA

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 27.

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 29