Posts

Showing posts from March, 2024

HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 31

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 31 Ilipoishia………. Elvine alipoteza amani kuliko hata mkewe maana kila alipomtazama mkewe basi moyo wake ni kama ulikuwa unachomwa na mwiba uliojishikiza huko kwenye mishipa ya moyo. Nafsi yake ilitaabika na ndipo alipoamua kutafuta muda mzuri, baada ya chakula cha jioni, azungumze na mkewe, maana ule ukimya wa siku mbili ulikuwa adhabu kubwa sana kwake. Kusoma sehemu ya 30 bonyeza hapa Sasa inaendelea………. Elimina mamy naomba kujua kwanini hutaki kuniuliza kuhusu sababu ya haya yote? Maana najua unajua kuwa kuna mahali mimi nilikosea, sasa unapokaa kimya hivyo… kiukweli unazidi kunichanganya maana ni kama hutaki kujua, sasa unadhani mimi roho yangu itatulia kweli?. Hata kama ungekuwa wewe lazima usingepata amani, ungekuwa hata unawaza hivi nakuwaziaje, nakuonaje na ninajisikiaje ninapokuona, sasa kwanini wewe umekaa kimya, sema neno tafadhali? (Elvine alikuwa akiongea bila kumtazama mkewe usoni maana moyo wake haukuwa katika hali ya utulivu). Pamoja na ...

SIMULIZI YA KUFURAHISHA, “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”. SEHEMU YA 17.

Image
HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA KUMI NA SABA Ilipoishia.... Siku moja akiwa amelala aliota moto mkubwa unawaka ndani ya maji lakini ule moto ni kama unaofifia kwa kuzidiwa na yale maji. Alipoamka akaikumbuka ndoto aliyowahi kuota utotoni ikamkumbusha kuwa hatakiwi kuzima namna hiyo na akajikuta kakumbuka sana vile viusumbufu vya kivita na maadui. Lakini hakujua kumbe kuna bomu kubwa kaandaliwa.....  Kusoma sehemu ya 16 bonyeza hapa. *.   *.    *.   *.    *.    *.   *.  Elvine alikuwa ameketi juu ya mti katikati ya poli fulani akiwa na amani sana. Akiwa pale aliweza kuona umbali mrefu sana. Alishangaa baada ya kumuona mtoto wa kiume mwenye umri kama wa miaka 7 hivi anazunguka zunguka mule polini. Akacheka sana halafu akasema "Kuna vitoto vya ajabu Duniani jamani. Sasa angalia huyu mtoto anataka nini huku polini muda huu?" Akatabasamu akachuma embe lililoiva kwenye ule mti na kuanza kulila. Yule  mtoto alikuwa akijiimb...

SIMULIZI YA KUFURAHISHA, “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”. SEHEMU YA 16.

Image
  SIMULIZI YA KUFURAHISHA, “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”.   SEHEMU YA 16.  Ilipoishia.....      Sherehe zilianza na watu wengi sana walikuja tena wachungaji walikuwa wengi sana. Elvine alifurahi baada ya kumuona baba yake na mama yake wamekuja tena wakiwa wazima wa afya. Elvine pamoja na kufurahi lakini bado alikuwa na wasiwasi  k usoma sehemu iliyopita bonyeza hapa. Sasa inaendelea.... Alitazama Elimina namna alivyopenda akasema kimoyomoyo 'hakika malkia wangu usife mapema bado natamani kuona ulipendeza hivihivi daima'. Wakaingia kanisani ambapo aliyesimamia ibada ya send-off alikuwa ni mchungaji wa kanisa jilani. Lakini Elvine alikuwa na wasiwasi sana na yule mchungaji maana tangu alipofika alikuwa hawatazami watu usoni bali mda mwingi alitazama chini kama anayetunza sheria za familia.  Elvine hakutaka kujaji saana lakini kuna namna alimkazia macho sana yule mchungaji maana kwa mauzauza tu yanayomuwinda aliona ni lazima amchunguze kila mtu ana...

Popular posts from this blog

MAAJABU YA AKIBA

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 29

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 27.