Posts

Showing posts from September, 2025

UKIJUA HILI KUHUSU WATU UTAFANIKIWA SANA.

Image
  UKILIFAHAMU HILI KUHUSU WATU  UTAISHI VYEMA SANA MAISHANI. Kuna ujuzi mwingi muhimu ambao kila mtu anapaswa kujifunza ili kufanikiwa maishani: mauzo, masoko, fedha, utatuzi wa matatizo, mawasiliano, majadiliano, na mengine mengi. Lakini kuna ujuzi mmoja ambao ni zaidi ya hazina—ukiupata, unafungua milango mingi bila hata kugonga. 👉 Ujuzi huo ni KUWAFAHAMU WATU. Ukifanikiwa kuwafahamu watu—saikolojia yao, hisia zao, na namna wanavyotaka kutendewa—hakuna mahali utakwamia. Kwa nini? Kwa sababu kila kitu unachokitaka kipo mikononi mwa watu: fedha, ardhi, bidhaa, mitaji, fursa, ushirikiano, na huduma zote. Kwa kifupi: 👉 Mahusiano mazuri na watu ni bidhaa ADIMU yenye thamani kubwa sana. Na kama ni bidhaa, basi lazima ujifunze namna ya kuitengeneza, kuikuza na kuitunza. Katika sanaa hii ya kuishi na watu, kuna sheria mbili kuu zinazokuongoza. SHERIA YA KWANZA: THE GOLDEN RULE Kanuni hii inasema: “Watendee wengine kama unavyotaka kutendewa wewe.” Hii ni kanuni nzuri s...

HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 31

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 31 Ilipoishia………. Elvine alipoteza amani kuliko hata mkewe maana kila alipomtazama mkewe basi moyo wake ni kama ulikuwa unachomwa na mwiba uliojishikiza huko kwenye mishipa ya moyo. Nafsi yake ilitaabika na ndipo alipoamua kutafuta muda mzuri, baada ya chakula cha jioni, azungumze na mkewe, maana ule ukimya wa siku mbili ulikuwa adhabu kubwa sana kwake. Kusoma sehemu ya 30 bonyeza hapa Sasa inaendelea………. Elimina mamy naomba kujua kwanini hutaki kuniuliza kuhusu sababu ya haya yote? Maana najua unajua kuwa kuna mahali mimi nilikosea, sasa unapokaa kimya hivyo… kiukweli unazidi kunichanganya maana ni kama hutaki kujua, sasa unadhani mimi roho yangu itatulia kweli?. Hata kama ungekuwa wewe lazima usingepata amani, ungekuwa hata unawaza hivi nakuwaziaje, nakuonaje na ninajisikiaje ninapokuona, sasa kwanini wewe umekaa kimya, sema neno tafadhali? (Elvine alikuwa akiongea bila kumtazama mkewe usoni maana moyo wake haukuwa katika hali ya utulivu). Pamoja na ...

Popular posts from this blog

UKIJUA HILI KUHUSU WATU UTAFANIKIWA SANA.

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 29

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 27.