HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 23.

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 23. Ilipoishia...... Alipofika nje, alimkuta Elimina katahamaki sana tena anahasira sana.  "Umefanya nini Elvine? Elimina aliuliza kwa ukali sana tena hadi macho yalikuwa mekundu kama damu kwaajili ya kujaa hasira.... Swali; kwanini Elimina anahasira? Na Elimina huyu anasiri gani na nyumba iliyoungua moto? Kusoma sehemu ya 22 bonyeza hapa   Sasa inaendelea...... Elvine alikuwa anatetemeka  kwa hofu ya yale anayoyaona lakini alistaajabu kuona ni kama mkewe hajali sana kuhusu yeye. Alimtazama kwa makini sana mkewe akiwa anajaribu kutafakari kwanini anaonekana kuwa na hasira juu yake. Elimina akajishitukia "Hey, wewe! Nini sasa unanitazama hivyo?" "Nakutafakari sipati majibu!' "Nimefanyaje kwani?" "Hamna ila sijajua kama umenihofia mimi au hilo swali lako linamaana gani? "Elvine baba sina maana hiyo uliyoelewa wewe kabisa. Shida yangu mimi umefanya nini mpaka unataka kuhatarisha maisha Yako namna hii. Hujui namna ga

HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 19

 



HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 19

Ilipoishia....

Katikati ya ule moshi walionekana watu wawili wanatembea kuingia ndani ambao walikuwa mwanaume na mwanamke, wenye sura za tabasamu zilizojaa chuki, mateso pasipo huruma na furaha Kwa wengine. Lakini ni ajabu maana walipoingia walikuwa  watu wanaofahamika sana na ni ajabu kuwafahamu....

kusoma sehemu ya 18 bonyeza hapa

Inaendelea....

Alionekana binti mmoja mrembo kapendeza mno kwa mavazi yake mekundu kwanzia juu mpaka chini. Yaani, gauni refu jekundu lililokuwa likitambaa mpaka chini renye maua ya kuvutia sana, viatu vyake virefu vyekundu ambavyo kama hujawahi vaa viatu virefu basi viatu vile huwezi kuvitumia kwa majaribio kabisa, kichwani alibana nywele zake ndefu kwa kibanio chekundu na mikononi alivaa bangili mbili za rangi nyekundu pia, ni wazi kusema kwamba alipendeza mno na hakuvaa kimaskini hata kidogo maana mavazi yake kwa makadirio ya haraka labda yalikadriwa laki tano au sita ili mtu kuyamiliki.

Alikuwa kashikwa mkono na kijana mmoja ambaye ni wazi alikuwa kamzidi kiumri yule binti. Sura ya Binti yule ilikuwa inang'aa sana na kadri aliposogea jukwaani ndipo alipozidi kung'aa zaidi.

Walipanda jukwaani ndipo hali ya pale ndani iliporudi kama ilivyokuwa  awali. Yaani, watu wakaacha kukohoa na moshi ukatoweka. Mtu mmoja ambaye ndiyo alikuwa kama muendesha hafla ile yaani MC akasimama mbele ya jukwaa na kuwakaribisha wageni hao ambao ndio walionekana ni muhimu sana katika tukio hilo, Kisha akawaamuru watu wakae na kuachia jukwaa chini ya uongozi wa wageni walioingia.

Yule kijana wa kiume alisimama na kutabasamu na kuanza kutoa hotuba yake.

" Ni muda mrefu sana sijatoka kuona Dunia inavyoenda lakini sasa nadhani ni nafasi yangu ya kuisumbua Dunia na Elvine lazima nimnyooshe kidogo japo ni mpendwa wangu. Leo ninafuraha sana maana binti yangu kaanza kuonesha ujuzi alioupata masomoni unafanya kazi kwakweli makofi kwake! (Wote wakapiga makofi).

Akaendelea; "Mimi kama baba wa Erijini nataka kufanya mambo kama navyoagizwa na makao makuu bila makosa kabisa. Mimi kukabidhiwa nyie niwaongoze ni kwaajili ya hatima ya huyu binti maana bila yeye kuzaliwa mimi nisingeaminiwa kuongoza kundi hili. Nataka mjue kitu kimoja Kwa sasa kikundi cha powers kinaenda kupata nguvu zaidi maana binti yangu kakamilisha masomo na yupo tayari kwa kazi na hakuna wa kumzuia. Erijini njoo binti yangu useme neno.

Binti alisogea pale alipo baba yake, kwa kuwatazama kwa haraka ni vigumu kuamini kama ni mtu na baba yake maana nyuso zao hazikuonesha kutofautiana sana. Erijini alitembea kwa madaha sana na akabadilisha macho yake kuwa mekundu kama damu kisha akaanza kucheka bila sababu tena Kwa sauti kubwa. Alipofika mahali baba yake kasimama akamkumbatia na kumwambia "Bado muda kidogo tu namalizia kazi ulionipa baba" alipomaliza kusema alipaa hewani bila mabawa na kusimama juu kabisa mahali pasipo na chakusimamia na yote aliyafanya kuwaonyesha wale watu namna gani anauwezo mkubwa sana.

Alisimama Kwa muda kisha akabadilisha mazingira ya pale ndani na kupafanya paonekane tofauti kabisa na mwanzo yaani kila kitu kilibadili rangi yake na kuwa nyeupe sanaa. Mara hii pale mbele hapa kuwa na jukwaa ila madhabahu iliyofunikwa na shuka jekundu. Yaani, kila kitu kilikuwa cheupe isipokuwa hiyo madhabahu pekee. Viti havikuwepo tena kama mwanzo. Wote walishangaa na kuanza kumpigia makofi yule binti.

Erijini baada ya kufanya hayo alishtuka kutoka juu alipokuwa kaganda hewani kisha akatua juu ya Ile madhabahu ambayo baada ya yeye kuisimamia tu ilianza kuwaka moto na ndipo ukumbi mzima ukasema "MOTO KWA MOTO, DAMU KWA DAMU" Kisha watu wote wakapiga magoti na kumsujudia yule binti kuonyesha wamekubali na wapo tayari kutawaliwa. Yule kijana wa kiume ambaye ni baba wa Binti yule alitabasamu na kutikisa kichwa ishara ya kufurahishwa na uwezo wa mwanae.

Binti aligeuka na kumtazama baba yake Kisha akasema "baba I shall win the battle before the battle wins me" yaani atashinda vita kabla vita havijamshinda. Baba alitabasamu tu.

Binti alianza kuongea na kuwaambia wale watu " Mimi ni Erijini lakini mtaani naitwa Erika na nimefanikiwa kuzizuia nguvu zangu kuonekana mbele ya Elvine na kwa sasa nipo kwenye hatua nzuri maana nakaribia kushinda moyo wake na nikifanikiwa hilo basi hatuna kikwazo kingine kwenye mambo yetu. Kuzaliwa kwangu kupitia Efraim ambaye Dunia inamtambua kama mfu kutaleta mabadiliko katika ufalme wa kishetani yaani, lazima lengo la baba yangu kuletwa huku nilikamilishe ili awe huru pia maana kafungwa muda mrefu kwaajili ya Elvine na amefungwa mpaka mimi nimekuwa sasa na leo yupo nusu huru. Uhuru wa baba yangu Efraim mimi ntaukamilisha kwa kulifanya kazi hii kwa ujuzi wangu wote.

Watu wote wakashangilia kana kwamba kuna mashindano ya Simba na yanga mule ndani. Baada ya muda waliruhusiwa kila mmoja kuondoka, hivyo wakaanza kuondoka pale ndani na baada ya muda pakawa patupu bali Erika tu na Efraim ndio walibakia pale ndani. Efraim akamwambia binti yake kuwa yeye hawezi kukaa na binti yake mpaka pale atakavyotimiza kazi aliyopewa. Wakati wanaendelea kuongea Efraim alifungwa na kamba ambazo hazikujulikana zilipotokea na kisha akatoweka.

Efraim alijikuta sehemu iliyokuwa inatisha zaidi maana huko kulikuwa ni kama chini ya mlima wenye volcano maana moto ulikuwa kila mahali na hapo alikuta kiti ambacho alikuwa akikalia miaka mingi sana kama kifungo na hakutakiwa kutoka hapo na ndipo alipokumbuka namna alivyochukulia.

Alikumbuka kuwa akiwa mdogo alikuwa rafiki wa Elvine na walipendana sana na kipindi hicho alianza kuota ndoto za ajabu ajabu sana mara yupo polini na watu asiowajua mara yupo barabarani anashuhudia ajali n.k. lakini hakujali pengine kutokana na utoto alionao alihisi ni ndoto tu za kawaida. Akakumbuka siku ambayo aligongwa na gari kwa makusudi na watu ambao lengo lao ilikuwa ni kumuuwa Elvine lakini hawakuwa wanamfahamu Elvine hivyo wakamuuwa yeye, lakini ukweli ni kuwa hawakumuuwa hata na ulikuwa mpango kamili wa mashetani kutaka kumtumia yeye hivyo Ile siku aligongwa lakini alijikuta sehemu nyingine kabisa na hakujua kafikaje. Akiwa huko alioneshwa namna watu wanavyolia kwenye msiba wake na akaambiwa hatoruhusiwa kuwa huru kutoka kwenda kuzurura Duniani mpaka atakapofanikiwa kupata mtoto ambaye atapewa nguvu za kishetani na kumuangusha Elvine. Mtoto alipatikana baada ya yeye kupewa mke ambaye ni jini na baada tu ya mtoto kuzaliwa yule jini aliteketezwa. Efraim aliishi ile sehemu ya kutisha pasipo ndugu wala rafiki bali mtoto wake tu ndio aliyekuwa anakuja kumuona na wala hakuishi naye pia maana Erijini alikuwa anakaa kwenye chuo cha mafunzo maana alitarajiwa kuja kufanya kazi moja tu ya kumuangamiza Elvine na wote ambao ni watumishi wa Mungu wenye uwezo mkubwa wa kuwasumbua.

Miaka ilipita mingi sana na sasa mtoto wake kakua na kaanza kazi aliyopewa maana aliambiwa kuwa mtoto huyo akimuangusha tu Elvine basi yeye atakuwa huru. Efraim alikuwa tayari kapandikizwa roho mbaya ndani yake kwahiyo aliona ni sawa apotezwe na alikuwa akimfundisha binti yake mbinu za kumfanya Elvine afurahi maana yeye alikuwa anajua vitu ambavyo Elvine anapenda toka utotoni mwake. Kwahiyo kazi kubwa aliyokuwa nayo yeye na Erijini yaani Erika ni kumuangusha Elvine.

Ilikuwa ni vigumu Elvine kuona ushetani ndani ya Erika maana Erika alipokuwa anaenda Kwa Elvine alikuwa anajua nguvu zote alizonazo kwahiyo hakuwa hata na chembe ya nguvu za kishetani ndani yake ila hurudi kuubeba uwezo wake pindi akitoka kuonana na Elvine.

*.      *.         *.           *.       *

Elvine alikuwa akimpenda sana Erika na kwake alimfanya kama mdogo wake. Elimina hakuwa anajua sana urafiki mkubwa uliojengwa kati ya mumewe na Erika. Siku moja Elimina aliota ndoto ambayo bila shaka ilikuwa ni kama onyo kwa Elvine maana aliota kuwa shati la Elvine linaungua. Alipojaribu kumsimulia Elvine, Elvine hakujali maana alikuwa anajiamini sana kuwa ananguvu za Mungu sanana Mungu hawezi kumuacha.

Siku moja Erika alikwenda nyumbani kwa Elvine na alipofika aliwakuta Elvine na mkewe sebuleni wamekaa wanakula. Alipofika alikaa pembeni yao na stori zikaanza ambapo. Wakati wanaongea Erika akauliza "hivi hii nyumba mbona sijaona vitoto vinacheza shida nini?" Kwa namna alivyo mropokaji hakuna aliejaji sana lakini neno lile likaingia moyoni mwa wanandoa wale.

Erika alipoondoka Elvine akamuuliza Elimina "hivi ni lini na mimi nitaitwa baba?" Aliuliza hivyo akiwa katika namna isiyo ya utani kabisa. Elimina alitabasamu na kusema "wakati wa Bwana"

"Hiii!! Elimina hivi unautani eeh? Mimi natamani niitwe baba sasa khaa!"

"We si unaimani kubwa! Kwanini usimuombe Mungu wako afanye jambo"

"Ety eeh!? Ndio unaniambia mimi hivyo?"

"Ni kosa?." Wakati mabishano yasiyo rasmi sana yanaendelea kati yao. Elimina aliingiwa na malaika wa Bwana palepale na Elvine hakujua. Elimina akaanza kuongea maneno ambayo ki uhalisia sio yeye alikuwa alisema ila ni aliye ndani yake.

"Masikini Elvine! Umetulia! Wala huoni mbele! Umekunja mikono wala hutaki kufanya kazi uliyoitiwa. Unatamani ufanyiwe na Mungu mambo mengi lakini je wewe umefanya nini? Kamwe Mungu hawezi kukupa mwana kama huwezi badilika. Ataharibu uzao wote tumboni mwa Elimina kamwe huwezi pata uzao"

"Unaongea nini wewe?"

Sijui na wala sifahamu naongea nini lakini jitahidi kumtafuta Mungu tena. Rudi kwenye njia, kafanye kile Mungu anataka, acha kazi unayofanya maana sio yako. Fanya maamuzi haraka maadui zako wako mbioni kukuangamiza. NI ONYO!" Elimina alikuwa anaongea hayo maneno Kwa upole sana jambo ambalo lilimfanya Elvine kutambua kuwa yele sio Elimina ila kuna anaeongea ndani yake. Lakini Elvine alikuwa anaipenda kazi yake, anapenda kuitwa meneja, anapenda kuonekana bosi, sasa akiwaza kuhusu kuwa mchungaji anaona kama hailipi kabisa japo alikuwa anapenda sana kuwa mchungaji zamani. Alijiwazia mwenyewe kisha akaamua kuondoka pale sebuleni maana aliona anazidi kuchanganywa na maneno ya mkewe. Aliingia chumbani kwake ambako alishangazwa baada ya kumkuta mtoto mchanga analia kitandani kwake......

"Huyo mtoto ni nani na katoka wapi? Fatilia sehemu inayofuata..."

Kusoma sehemu ya 19 bonyeza hapa.

Simulizi  hii imendaliwa na kuandikwa na JACQUELINE JOHN.

Mtunzi wa Hadithi (simulizi) .

 Mawasiliano:

Whatsapno. >>>>> +255789523850. Normal >>>>>+255747313148.

                            &, 

Imehaririwa na MIGONGO ELIAS. Mhariri.

Mawasiliano:

Whatsapno. >>>>> +255767653697. Normal >>>>>+255783327456.

                        GeT tO tHe NeXt LeVeL!

Kama umejifunza kitu shiriki nasi katika comment hapo chini, ili kuboresha na kujifunza zaidi.

 

 

 

 

 

Popular posts from this blog

GHARAMA 5 ZA KUUFIKIA UKUU UNAOUTAKA.

USIKUBALI KUAJIRIWA KABLA HUJASOMA HAPA.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.