LEVEL ZA MAFANIKIO SEHEMU YA TANO.

Image
  LEVEL ZA MAFANIKIO SEHEMU YA TANO. Baada ya kufika Investor Level, ambapo pesa zinaanza kufanya kazi kwa ajili yako kama tulivyoona somo lilopita boss. Sasa kuna hatua ya mwisho ya juu zaidi ambayo watu wachache sana duniani wanaifikia kwa ufahamu na nidhamu kali sana, hii si nyingine bali ni: FREEDOM LEVEL ( HATUA YA UHURU WA KWELI) HII SIYO TENA LEVEL YA PESA TU, KAMA ZILE LEVEL ZINGINE. Boss hapa siyo swali la: una pesa kiasi gani una biashara ngapi, una assets kiasi gani? 👉 Hapa swali ni moja tu: UNAISHI MAISHA UNAYOYATAKA? Unajua kila mtu qnamatamanio yake, namna ya lifestyle yake, kuna vitu anapendelea kuvimiliki, lakini sasa ni wacahche wanaosatify wengi wanaishia kutamani tu boss. MAANA HALISI YA UHURU HUU Freedom level ni pale ambapo: ---- Hufanyi kitu kwa sababu unalazimika kufanya. 👉 Yaani, Unafanya kwa sababu unachagua kufanya. Sijui kama unanipata? AINA 4 ZA UHURU KATIKA LEVEL HII 1. UHURU WA MUDA Unaamua: uamke saa ngapi, ufanye nini, uishi wapi, uen...

HUWEZI KUBADILIKA BILA KUJITAMBUA.


HUWEZI KUBADILIKA BILA KUJITAMBUA.

Watu wengi hutamani kubadilisha maisha ya tabia, kipato, mahusiano, au jinsi wanavyojiona. Wengine husoma vitabu, huhudhuria semina, na kuweka malengo mapya kila mwaka. Lakini, pamoja na juhudi zote hizo, hujikuta wakirudia hali ileile.

Sababu si kukosa bidii, no. Mara nyingi ni kukosa #KUJIJUA wao kama wao.

Kujiboresha bila kujitambua ni kama kujenga bila ramani.

Unapojaribu kubadilika bila kuelewa wewe ni nani, unaishia kuiga maisha ya wengine tu. Utaweka malengo yasiyoendana na hali yako, uwezo wako, au hali yako ya ndani.

Ndiyo maana baadhi ya malengo huonekana mazuri kwa macho ya watu, lakini moyoni hayana uzito wowote. Unapoanza kuchoka haraka, si uvivu tu, wakati mwingine ni ishara kwamba njia uliyopo siyo yako.

Kujitambua kunahitaji ujasiri wa kukubali ukweli kuhusu wewe.

#Kujitambua siyo kujipongeza kila wakati. Ni kukubali ukweli wote mtamu na mchungu.

Ni kuona #NGUVU zako bila kiburi, na #UDHAIFU wako bila kujilaumu. 

Ni kujiuliza maswali magumu kama: Mimi ni nani? Ninakwenda wapi? Kwa nini narudia makosa yaleyale? au Ni hofu gani inaniongoza bila kujua?

Huwezi kurekebisha kile ambacho hujakikubali.

Kujitambua huzaa mabadiliko ya kudumu

Unapojifahamu, maamuzi yako yanabadilika. Unaacha kuishi kwa mazoea na kuanza kuishi kwa #MAKUSUDI.

Unaacha kuhiuliza, “Watu watasemaje?” na kuanza kuuliza, “Hili linaendana na mimi?”

Mabadiliko yanayotokana na #SAUTI na #UELEWAwa ndani hudumu kwa sababu yanajengwa juu ya #UKWELI, si msukumo wa muda mfupi tu!.

Namaliza kwa kusema,

Kama kweli unataka kubadilika na kubadilisha chochote kwenye maisha yako, anza kwa kujifahamu wewe kwanza. Kaa kimya mara kwa mara tafakari, jisikilize kitokea ndani yako, na ukubali ukweli wako bila #KUHOFIA WALA #KUKIMBIA.


Kujitambua si mwisho wa #SAFARI—ni mwanzo wa #MABADILIKO ya #KWELI. Chukua muda mchache ujiulize swali hili:

Ni eneo gani la maisha yangu najidanganya

 mwenyewee na ninahitaji mabadiliko gani?


Add Value Network 

Migongo Elias 

#SeeYouNextLevel

Popular posts from this blog

UKIJUA HILI KUHUSU WATU UTAFANIKIWA SANA.

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 27.

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 29