MALENGO 6 YA ELIMU YANAYOWEZA KUBADILISHA MAISHA YAKO KABISA.

Image
  MALENGO 6 YA ELIMU YANAYOWEZA KUBADILISHA MAISHA YAKO KABISA. Watu wengi wanaposikia neno elimu, jambo la kwanza linalokuja akilini ni: shule, mitihani, vyeti, Pesa au ajira. Asilimia kubwa jamii yetu inaamini sana katika ajira, kwamba ukiwa msomi/ mwenye elimu huku hujaajiriwa unaonekana si lolote wala chochote. Lakini ukweli ni kwamba elimu ni kubwa zaidi ya hayo. Boss, elimu siyo tu kukariri taarifa darasani au kupata alama nzuri kwenye mtihani ndugu yangu. In short boss, Elimu si karatasi ya cheti tu, bali ni mchakato wa kumjenga mwanadamu kamili. Hapa namaanisha kuwa, Elimu ya kweli ni mchakato wa kumjenga mtu kiakili, kiuchumi, kijamii, kiutamaduni na kimaadili ili aweze kuishi maisha yenye maana na mchango kwa jamii. Kwa kifupi boss, elimu inapaswa kumbadilisha mtu kutoka alivyo leo na kumpeleka katika kiwango bora zaidi cha maisha yake na yawatu wanaomzunguka. Kitu hiki ndo kimenisukuma leo tuangalie malengo makuu sita ya elimu kwa mtu husika boss. 1. KUKUZA AKIL...

KUJILINGANISHA NI SUMU HATARI.


 KUJILINGANISHA NI SUMU HATARI.

Tatizo kubwa la kizazi hiki si kukosa UWEZO binafsi.

Bali ni KUJILINGANISHA kupita kiasi.

Hebu tazama kwa mfano, nafungua simu yako, unaona maisha ya wengine, yanaonekana yamepangwa.

Wamefanikiwa.

Wanasafiri.

Wanaonekana kuwa na furaha sana.

Wanavaa na kula vizuri.

Halafu unaanza kujiuliza:

“Mimi niko wapi?” mara unasema mimi si chochote.

Mdogo mdogo, unajikuta unapima thamani yako kwa vipimo vya watu wengine. Hapo ndipo tatizo linapo anzia.

Lakini ukweli ni huu; 

๐Ÿ‘‰ kila mtu ana safari yake, kila mtu anasababu yake. Ambayo yaweza kuwa nitofauti kabisa na wengine.

Kuna anayekimbia haraka kwa sababu alianza mapema.

Kuna anayepanda polepole kwa sababu anajenga msingi imara.

Kuna anayeficha mapambano yake nyuma ya picha nzuri.

Usilinganishe mwanzo wako na mwisho wa mtu mwingine.

Si unajua maisha ni kama kitabu, ukurasa wako wa kwanza una weza kuwa ni wa mwisho kwa mwingine. Kila mtu anakitabu chake na kurasa zake.

Maisha yako hayakuitwa KUIGA watu wengine, bali kuishi KUSUDI lako.

Vipaji vyako ni vya kipekee.

Uwezo wako ni wakipekee.

Wakati wako ni wa kipekee.

Safari yako ina maana yake.

Badala ya kuangalia wengine wamefika wapi, jiulize:

๐Ÿ‘‰ Leo nimekua kiasi gani kuliko jana?

๐Ÿ‘‰ Nimejifunza nini leo?

๐Ÿ‘‰ Ninakaribia kiasi gani ndoto yangu?

Kumbuka;

Wakati unajilinganisha, unapoteza amani.

Kujlinganisha ni mwizi wa muda.

Mara tu unapojilinganisha unapoteza NGUVU, THAMANI YAKO NA UWEZO WAKO WA KUFIKRI.

Lakini ukiacha kujilinganisha, kimya kimya utaanzq  kujithamini, unapata nguvu, furaha, amani, kujiamini, kutumia uwezo wako na mengine kibao yafananayo na hayo.


Hivyo basi;

Tambua wewe ni nani, UDHAIFU na UIMARA  wako ni upi. Wekeza sana kwenye UIMARA wako.

Kisha pambana mdogo mdogo #MAISHA yanajengwa na kuandaliwa siku moja na wee utafika huko.

Baini, uko wapi unataka nini na unaenda wapi?. Heshimu hatua zako unazopiga kidogo kidogo.

Heshimu mwendo wako.

Heshimu historia yako.

Kwa sababu wewe sio wao.

Na wewe haukuitwa kuwa wao.

Wewe uliitwa kuwa wewe halisi. Yes wewe Orginal.๐Ÿ’™๐Ÿ”ฅ

Kama umejifunza kitu tuandikie kwa comment.

Kujifunza zaidi bonyeza hapa

Migongo Elias 

Add Value Network 

#knowledgeispower 

#seeyounextlevel

Popular posts from this blog

UKIJUA HILI KUHUSU WATU UTAFANIKIWA SANA.

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 27.

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 29