INUKA TENA

Image
  INUKA TENA Siku zote maisha siyo safari ya watu wasiopata changamoto. Ni safari ya watu wanaoanguka, wanajifunza, na kuinuka tena kwa nguvu zaidi boss. Watu wengi hudhani mafanikio ni safari ya moja kwa moja the straight line ambapo: unafanya vizuri kila wakati, hakuna kushindwa, hakuna maumivu. Lakini ukweli ni kwamba, kila mtu aliyefanikiwa amewahi kuanguka mara nyingi zaidi kuliko unavyofikiri boss. Tofauti yao na wengine si kwamba hawaanguki, noo, bali ni kwamba waliinuka tena baada ya kuanguka. BOSS, KUANGUKA SI MWISHO WA SAFARI. Kuanguka ni sehemu ndogo tu ya ukuaji. Kwasababu Unaposhindwa: unajifunza kitu kipya, unagundua makosa yako, unaelewa njia iliyo bora zaidi. na unapata uzoefu ambao hauwezi kufundishwa darasani ndugu yangu. Tatizo la watu wengi hufanya kosa moja kubwa: yaani,  wanaona kuanguka kama mwisho wa safari yao, mara wao ni wakushindwa tu. Wao si lolote. Hapo ndipo ndoto nyingi hufa kabla hazijakomaa kabisa ndugu. Sikiliza boss, Kuanguka haku...

SIYO PESA PEKEE ZINAZOKUFANYA UWE MWEKEZAJI, NI MISINGI.

 


SIYO PESA PEKEE ZINAZOKUFANYA UWE MWEKEZAJI, NI  MISINGI.


Watu wengi wanapofikiria UWEKEZAJI, jambo la kwanza linalokuja akilini mwao ni pesa nyingi.
Ndiyo maana wengine husema, “Nikishapata pesa nyingi ndipo nitaanza KUWEKEZA.”.

Lakini ukweli ni tofauti kidogo.
Uwekezaji wa kweli hauanzi na pesa nyingi.
Unaanza na MISINGI sahihi ya KIFEDHA.
Watu wengi hupata na kuzalisha pesa siyo tatizo kwao, lakini hawajengi utajiri.

Kwa nini?
Kwa sababu hawajajifunza misingi ya kuitunza na kuikuza. Kila kitu kina misingi na kanuni zake.
Kabla ya kufikiria uwekezaji mkubwa, jifunze kwanza mambo machache ya msingi.

Jifunze kuishi chini ya kipato chako.
Jifunze kuokoa hata kama ni kidogo.
Jifunze kupanga matumizi yako.
Na jifunze kuwa na subira.
Kwa sababu uwekezaji si mbio za haraka.

Ni safari ya uvumilivu.
Ni kama kupanda mti.
Unapanda mbegu leo.
Unaimwagilia kila siku.
Unaipa muda ikue.
Halafu baada ya muda, inaanza kutoa kivuli  na baadaye matunda.

Tatizo la wengi ni kutaka matunda kabla ya kupanda mbegu na kuimwagilia
Lakini ukweli unabaki kuwa huu:

👉 utajiri wa kudumu hujengwa kwa uwekezaji na uwekezaji hujengwa juu ya misingi imara.
Hata kama unaanza kidogo leo, usidharau hatua hiyo.
Kila akiba ndogo ni mbegu.
Kila uamuzi mzuri wa kifedha ni maji ya kumwagilia mbegu hiyo.
Na kadri muda unavyopita, mbegu hiyo inaweza kukua na kuwa mti mkubwa.
Anza pale ulipo.
Anza na kile ulichonacho.
Lakini hakikisha unajenga misingi sahihi ya uwekezaji.
Kwa sababu mwisho wa siku,
sio pesa nyingi zinazounda utajiri…
bali ni nidhamu ya kifedha inayojengwa taratibu.

Je, unachangamoto katika uwekezaji na unahitaji usaidizi?

Naamini umejifunza kitu kujifunza zaidi tembelea
https://addvaluetz.blogspot.com

Self Awareness (Kujitambua).
Investment (Uwekezaji).
Personal Development (Maendeleo binafsi).
Migongo Elias.
+255767653697
Add Value Network.
Knowledge Is Power.

Popular posts from this blog

UKIJUA HILI KUHUSU WATU UTAFANIKIWA SANA.

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 27.

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 29