Posts

Showing posts from May, 2024

HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 31

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 31 Ilipoishia………. Elvine alipoteza amani kuliko hata mkewe maana kila alipomtazama mkewe basi moyo wake ni kama ulikuwa unachomwa na mwiba uliojishikiza huko kwenye mishipa ya moyo. Nafsi yake ilitaabika na ndipo alipoamua kutafuta muda mzuri, baada ya chakula cha jioni, azungumze na mkewe, maana ule ukimya wa siku mbili ulikuwa adhabu kubwa sana kwake. Kusoma sehemu ya 30 bonyeza hapa Sasa inaendelea………. Elimina mamy naomba kujua kwanini hutaki kuniuliza kuhusu sababu ya haya yote? Maana najua unajua kuwa kuna mahali mimi nilikosea, sasa unapokaa kimya hivyo… kiukweli unazidi kunichanganya maana ni kama hutaki kujua, sasa unadhani mimi roho yangu itatulia kweli?. Hata kama ungekuwa wewe lazima usingepata amani, ungekuwa hata unawaza hivi nakuwaziaje, nakuonaje na ninajisikiaje ninapokuona, sasa kwanini wewe umekaa kimya, sema neno tafadhali? (Elvine alikuwa akiongea bila kumtazama mkewe usoni maana moyo wake haukuwa katika hali ya utulivu). Pamoja na ...

KWANINI UNAHITAJI PESA.

Image
  KWANINI UNAHITAJI PESA? Tunaishi kwenye dunia ambayo karibia kila kitu kina hitaji pesa. Chakula, maradhi, nguo na mengine kibao. Kama utaniazima dakika mbili za kusoma hadi mwisho ujumbe huu? Zitakuwa ni dakika 2 za matumizi bora kabisa ya muda kwenye maisha yako. Huta jutia bundle, muda wala nguza zako. Mara nyingi watu wakija kupata ushauri kwangu, kuhusu kupata pesa huwa siwajibu Kama walivyouliza. Wengi wao huuliza hivi, Mwl. nifanyaje ili nipate fedha zangu mwenyewe? Kama nilivyosema swali hili huwa silijibu kama lilivyo kusudiwa na waulizaji. Nami huwajibu kwa kuwauliza swali; KWANINI UNATAKA PESA? Kwa  bahati mbaya sana wengi huwa hawana majibu ya kueleweka ya swali hili. Wengine huseme ili nitumie tu, ili niinjoy maisha n.k. Nafahamu kabisa kuwa hata wewe unataka pesa. Ndiyo maana umeajiriwa, unafanya kazi, unakaba roba, unaomba, unalima n.k  moja ya sababu kubwa ya kufanya hivyo ni ili upate pesa. Si ndiyo rafiki!? Kama ndiyo napenda kukuuliza na w...

THANK DIFFERENT (FIKIRI TOFAUTI).

Image
  * THINK DIFFERENT"  (FIKIRI TOFAUTI) * . Ilikuwa kampeni kali na ya kuvutia iliyozinduliwa na Apple Computer ( Apple ) mnamo 1997. Kama ulikuwa umezaliwa tupungianeđź«· Ilidumu kwa miaka kadhaa na bado inachukua hatamu katika historia ya uuzaji na utangazaji.  Think Different"  ilikuwa na mafanikio makubwa. Ilisaidia Apple kujionyesha kama chapa kwa ajili ya watu wenye * UBUNIFU, * na wanaofikiri tofauti. kampuni iliyounga mkono ubunifu na kutofuatana na desturi za kawaida. Kampeni hiyo haikuzidisha mauzo tu bali pia ili kuza picha ya Apple kama chapa nzuri na inayotamaniwa na wengi. Hata wewe ni shahidi tukizungumza kuhusu, apple na huduma zake. " * Think Different" *   ni zaidi ya maneno tu; ni * FALSAFA. * kali. "Ni kuhusu umuhimu wa kufikiri bila kutegemea Mwawzo ya wengine, kupinga hali ilivyo, na kuamini kuwa watu binafsi wanaweza kuleta mabadiliko makubwa sana duniani." Rudia kusoma tena. Ndugu, kufikiri tofauti ni chanzo cha maba...

HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 26.

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 26. Ilipoishia.......... Alipomgeuza tu alishangaa kuona sura ya yule binti ni ya mbuzi. Aliogopa na kudondoka chini kwa kelele kuu alilia 'maaamaaaaaaa!!!!" Alijiokotaokota huku akiangukaanguka mpaka kwenye gari yake. Alipanda ndani ya gari na kuwasha gari. Alikimbiza gari mpaka akafika karibu na geti la nyumba ya Elvine, lakini kabla hajafika getini alishangaa kuona anaguswa mabegani ndani ya gari lake. Alitoa macho kwa uoga na mshtuko mkubwa mpaka akakosea njia na kwenda kugonga mti... Kusoma sehemu ya 25 bonyeza hapa. Sasa inaendelea......, Aligonga mti kwa nguvu mpaka naye akajipigiza kichwa kwenye usukani wa gari na gari ikaharibika sana upande wa mbele, alipona kwa neema tu kwa namna gari ilivyokuwa mwendo kasi angeweza hata kupoteza maisha lakini haikuwa hivyo. Alijikaza na kushuka kwenye gari akakimbia kuelekea kwenye nyumba ya Elvine,  njiani alikumbwa na kimbunga cha ajabu sana. Baada ya kile kimbunga kumpitia na kumzingazinga kwa muda ...

HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 25.

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 25. Ilipoishia...... "Ooh asante YESU maneno yako yamenipa na kiburi juu ya hawa watu, sahizi siwaogopi na wala hawaniwezi na Elvine lazima arudi haijarishi kwa namna gani? Nataka nimpe Mungu Sababu ya kumsaidia Elvine" Elimina akafuta machozi na akawa kajua aombe nini kwa sasa maana hataomba tena maombi ya kulalamika na maombi ya kwanini!! Akatabasamu alafu akasema " SASA VITA IANZE NAJUA SILAHA YANGU... Kama hujasoma sehemu ya 24 bofya hapa. Sasa inaendelea.... Elimina baada ya kujipa moyo akapata kiburi mbele ya hao maadui zake maana alijua umuhimu wake katika kumlinda Elvine. Aliamua kutoka pale ndani na kufuta machozi yake na akajisemea sasa sitalialia tena nimaombi ya vita mwanzo mwisho.  Aliamua kutoka na kwenda dukani kwake ili kuendelea na kazi zake. Ilikuwa imepita wiki sasa pasipo yeye kufika dukani kwake hivyo hata wateja walipungua maana kila walipokuja hawakumkuta. Alifungua duka lake akakaa nje ya duka mpaka jioni, japo alipat...

HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 24.

Image
HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 24. Ilipoishia.... " Baba nimeshakwambia, ufalme wa hawa wenzetu unanguvu kuliko sisi. Huoni mpaka sasa Elvine tunae, lakini bado mtu mmoja tu huko duniani anasababisha tusikamilishe mambo yetu?.  Hili swala linaniuma sana kuona tunafeli mbele ya hawa watu. Yaani kumpata Elimina sio kazi nyepesi, maana analindwa mno na ufalme wake na anamsimamo sana yule mwanamke.  Ila mimi nakuahidi baba naenda kumuangusha na akianguka, atalipia haya yote aliyoyafanya kwenye ufalme wa giza nasema atalipia, tena naapa ntafanya ajute na ajute tena labda asijichanganye" Erijini (Erika), aliongea kwa uchungu na hasira mpaka macho yakageuka rangi na kuwa rangi ya bluu.... Kusoma sehemu ya 23 bofya hapa. Sasa inaendelea.........  Efraim hakutaka kubishana sana bali aliamua kufanya sawasawa na hitaji la binti yake. Erijini alitoweka na kurudi Duniani kutoka kwenye ardhi iliyomficha Elvine Kwa kazi moja kubwa ya kumuangusha Elimina.  Elimina alikuwa haachi kuomba...

Popular posts from this blog

MAAJABU YA AKIBA

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 29

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 27.